Blogger Widgets 2012 | Mfaume Kikwato JR

PALACE HOTEL

PALACE HOTEL

Vumbua Hazina chini ya kizibo

Vumbua Hazina chini ya kizibo
+255788788218

BAYPORT

BAYPORT
KOPA BAYPORT

Saturday, December 29, 2012

JOSEPH CHAMELEONE ANUSURIKA KIFO SIKU YA BOXING DAY 2012


Msanii maarufu wa nchini Uganda Joseph Chameleone na mkewe Daniela, jana walinusurika kufa baada ya mtu mmoja kuvamia nyumba hiyo akiwa na Petroli kwa lengo la kumuua msanii huyo, lakini akiwa kwenye hazma ya kutekeleza tukio hilo moto wa Petroli aliotaka kuwachoma na ndani ya nyumba ya msanii huyo uli muunguza vibaya mtu aliyetaka kufanya tukio hilo

ALIYE JARIBU KUMUUA MSAANI WA UGANDA JOSEPH CHAMELEONE AFARIKI DUNIA

Mtu huyo aliye fariki masaa mawili yaliyo pita, Akipatiwa matibabu amefaamika kwa jina la Robert Kalamagi mwenye umri wa miaka 27, mkazi wa Seguku Kampala Uganda, amefikwa na umauti baada ya kujeruhiwa vibaya na moto wa petroli ambao alikuwa akijaribu kumwagia mke wa msanii huyo,

Daniela ambaye ni mke wa Chameleone, aliwaambia wa andishi wa Habari kuwa, Asubuhi ya Boxing Day alisikia vishindo sebuleni, wakati akiwa chumbani na alipojaribu kujua ninani, aligundua ni nani alimkuta marehemu na akajaribu kumuuliza anataka nini lakini akumjibu chochote, Alisema Daniela.


Aidha mke wa Msanii huyo alimuita Chameleone, ndipo mtu huyo alichukua geleni la lita tano kwa lengo la kumwagia Daniela, kinyume na matarajio yake petroli ilimwagikia yeye na alipo washa moto, aliungua kiasi cha kufanya mtu huyo kujeruhiwa vibaya na moto huo, Daniela anasema mtu huyo aliomba msaada alipokuwa anaungua na moto huo.


Kilicho washangaza watu wengi wa nchini Uganda ni baada ya mtuhumiwa kuwaeleza Polisi alipofanyiwa Mahojiano akiwa Hospitali kuwa, yeye ni shabiki mkubwa wa msanii huyo, na kilichotokea kwake alitumwa na mtu ilikumuua msanii huyo


Hatahivyo Polisi wa nchini humo wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo kubaini kama hilo nitukio la ujambazi au alitumwa na mtu kutekeleza tukio hilo

IAMOND AUKANA U FREEMASON, AWASHANGAA WANAOENEZA KUWA KABADILI DINI


Msanii anaye Ng'ara katika Tasnia ya Muziki wa Bongo Fleva hivi sasa, Diamond Plantum amekana kushiriki wala kujihusisha na imani inayousishwa na nguvu za giza ya "Freemason", na kusikitishwa sana na watu wanao sambaza maneno ya kuwa yeye amebadili dini.

"Mimi sijawahi kujiusisha na imani ya Freemason na wala sijui juu ya hilo kabisaa, Nimelelewa katika imani ya Kiislamu na ninacho juwa nikuwa Mungu ni mmoja....Siwezi Kuwa Freemason Hata siku moja"Alisema Diamond.


Akiongea na Campasvision Diamond, alisema Zaidi ameumizwa sana na kusikitishwa sana na habari zinazo zagaa kuwa yeye kabadili dini, kitu ambacho sio kweli..alisisitiza kuwa awezi kuiacha dini yake na kuwa na imani tofauti na aliyo lelelwa na kudai kuumizwa na watu wanao eneza habari hizo, Alisema Diamond


Vijana wanaoiga na Kukopi kazi zangu, kimsingi nafrahishwa sana tena inanipa nguvu yakuwa kazi zangu zinakubaliwa  hata nawasanii wenzangu, Swala ambali linanifanya niongeze juhudi zaidi katika kuboresha kazi yangu. Alisema Diamond


Akiongelea juu ya Video Mpya ya Kesho Diamond alisema, amefurahishwa sana na Wimbo huo kwani ni miongoni mwa nyimbo ambazo Mashahiri yake hayakumpa shida kutunga kabisa kwa ilikuwa kama masihara lakini kilichotoka nikitu ambacho kimesimama. Alimalizia Diamond

Tuesday, December 18, 2012

YANGA WATAMKUMBUKA YAW BERKO


SASA rasmi, Yaw Berko amebaki historia ndani ya klabu ya Yanga. Hiyo inafuatia klabu ya St Eloi Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kuridhika naye baada ya majadribio.
Katibu wa Yanga, Lawrence Mwalusako ameiambia KIKWATOJR.BLOSPOT.COM jana kwamba kipa huyo Mghana amefuzu majaribio Lupopo na amesajiliwa moja kwa moja.
Kuondoka kwa Berko, kunatoa nafasi kwa kiungo kutoka DRC, Kabange Twite kusajiliwa katika klabu hiyo ya Jangwani, akiungana na kaka yake, beki Mbuyu Twite. Wachezaji wengine wa kigeni wa Yanga ni kiungo Haruna Niyonzima kutoka Rwanda na washambuliaji Didier Kavumbangu kutoka Burundi na Hamisi Kiiza kutoka Uganda.
Berko alijiunga na Yanga SC mwaka 2009, akitokea Liberty Proffessional ya kwao Ghana, timu ambayo ilimuibua pia Michael Essein na nyota wengine kibao wa Ghana. Aliletwa nchini na kocha wa zamani wa Yanga, Mserbia Kostadin Bozidar Papic aliyewahi kupiga kazi Ghana katika klabu ya Hearts POf Oak.
Alikuwa kipa bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Bara msimu wa 2010/2011 na katika kipindi chake cha kufanya kazi Jangwani, anajivunia kuiwezesha timu kutwaa mataji ya ubingwa wa Bara msimu wa 2010/2011 na Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame mara mbili mfululizo, 2011 na 2012.
2011 alidaka mechi zote, lakini 2012 alidaka hadi Robo Fainali alipoumia na kumuachia Ally Mustafa ‘Barthez’ aliyedaka hadi ubingwa. Yanga imeridhika na uwezo wa Barthez langoni iliyemsajili kutoka Simba msimu huu na kuamua kuachana na Berko, ambaye alikuwa kipenzi cha wapenzi wa klabu hiyo.
Awali, Yanga ilijifikiria mara mbili kuachana na Berko, kwa kuhofia Barthez angeanza ‘kuwaringia’ kwa kuona amebaki peke yake kipa bora, lakini imepanga kumhamasisha Said Mohamed kuimarisha kiwango chake, vinginevyo atatemwa mwishoni mwa msimu.
Na Yanga imekuwa na ‘jeuri’ ya kumtema Berko baada ya kuona mwakani haitashiriki michuano ya Afrika, zaidi ya Ligi Kuu na jukumu la kwenda kutetea taji lake la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame mjini Kigali, Rwanda.
Japokuwa anaondoka, lakini kwa uhodari wake langoni, Berko atabakia kwenye kumbukumbu ya mashabiki wa Yanga.

WASIFU WAKE:
JINA: Yaw Berko
KUZALIWA: Oktoba 13, 1980
ALIPOZALIWA: Accra, Ghana
KLABU ZA AWALI:
Mwaka               Klabu
2000-2005:        Liberty Professional   
2005-2006:        Pisico Binh Dịnh F.C. (Vietnam, mkopo)  
2006-2009:        Liberty Professional   
2009- 2012:       Yanga SC
2012:                 St Eloi Lupopo 

Thursday, December 13, 2012

sharoo pengo lakoo bado haliwezi zibika mungu akubariki


Ni watu wengi wamehitaji kufahamu kuhusu kauli ya familia ya Marehemu mwigizaji/msanii Sharo Milionea baada ya tangazo la Airtel lenye sauti yake kuendelea kutumiwa na kampuni hiyo wiki kadhaa baada ya Sharo kufariki kwa ajali ya gari iliyotokea novemba 26 2012 Tanga.

Mjomba wa Marehemu ambae ndio msemaji wa familia Shaban Mkiete amethibitisha kwamba wamezungumza na kukubaliana na kampuni ya Airtel na hapa namkariri akisema “ni kweli tumekubaliana, kwa mujibu wa mkataba wao lilikua linaisha terehe 31 mwezi huu tumekubaliana kwamba liendelee kwa makubaliano ambayo tumekubaliana nayo sisi kati ya mzee Majuto ambae bado yupo na familia ya Marehemu, mama mzazi wa Sharo Milionea ameridhia hilo hakuna tatizo”

Siku ya msiba kikwatojr.blogspot.com ilipopata nafasi ya kuongea na mwakilishi wa Airtel alisema Marehemu Sharo Milionea alifariki ndani ya kipindi cha miezi 6 tu toka asaini dili la kuwa balozi wa Airtel na kufanya matangazo mbalimbali yeye na mzee Majuto.
                                     
Sio tu dili la Airtel, imefahamika tayari Sharo Milionea alikua amesaini mikataba mizuri na makampuni mbalimbali wakiwemo Wamarekani waliotengeneza filamu maarufu Afrika kama Yellow Card, Neria na nyingine ambapo kwa sasa Wamarekani hao wako hapa Tanzania na wametengeneza series kadhaa ikiwemo Wahapahapa na Siri ya Mtungi ambayo ndio Sharo Milionea kashiriki ndani na mpaka anafariki tayari alikua ameshaanza kucheza igizo hilo.

Monday, December 10, 2012

katika kuelekea sikukuu za x-mass na mwaka mpya viongozi mbalimbali wawatakia wananchi wao heri za sikukuu hizo

Mkuu wa wilaya ya mkinga mkoani Tanga Bi Mboni Mgaza wakati akiweka jingo katika Production za redio Mwambao Fm Tanga za kuwatakia mafanikio mema ya X mass na Mwaka Mpya wananchi wa wilaya yake ya mkinga

Hapa akiwa anapewa maelekezo na baadhi ya watangazaji wa redio mwambao fm jinsi ya kutia sauti za kuwatakia heri wananchi wa wilaya ya mkinga na mkoa wa tanga kwa ujumla.



picha ni Badhi ya watangazaji wa redio mwambao fm kuanzia kushoto ni Kalonga Kasati katikati ni mkuu wa wilaya ya Mkinga Bi Mboni Mgaza  wapili kutoka kwa mkuu wa wilaya ni Selemani Kibugo huku wamwisho ni kijana Almasi Shija  wakiwa katika picha ya pamoja mara bada ya kukamilisha mandalizi ya jingo za X Mass na Mwaka Mpya Kwa upande wa viongozi wa mkoa watanga kwa ujumla.

Mkurugenzi wa Blog ya kijamii ya Kikwatojr.blogspot.com anawatakia wale wote wanao tembelea blog hii ya kijamii kwa lengo la kupata habari mbali mbali na kimaendeleo Heri ya X Mass na Mwaka Mpya wadau wanguu wote nawapenda sana na nimewandalia mambo mazuri kwa mawaka wa 2013 cha msingi usisite kutembelea blog hii ya kijamii 

Saturday, December 1, 2012

Mali za Sharo Milionea zasalimishwa

Baadhi ya vitu vya marehemu Sharo milionea vilivyokamatwa baada ya msako mkali baina ya Polisi na wananchi wa Kijiji Songa Kibaoni vikiwa katika kituo cha polisi chumbageni  jijini Tanga.

vitu hivyo  vilivyoporwa na watu wasiojuliana katika ajali ya msanii mahiri wa 

filamu na muziki wa kizazi kipya nchini, Marehemu Hussein Mkieti ‘Sharo 

Milionea’ eneo la Songa Kibaoni wilayani Muheza mkoani Tanga, vimesalimishwa na wananchi wanaosadikiwa ni wezi.

Kwani alikuwa akitokea Jijini Dar es Salaam kuelekea kijijini kwao Lusanga 

Muheza, kwa dhumuni la kwenda kuwasalimia wazazi wake pamoja na kuwapelekea fedha za matumizi.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe, jana

 alithibitisha kupatikana vitu hivyo, ambako alisema upatikanaji wake ulitokana 

na msako mkali uliofanywa na uongozi wa serikali Muheza wakishirikiana na
Jeshi la Polisi wilayani humo.

Alisema kwamba baada ya kutokea kwa tukio hilo, Jeshi la Polisi mkoani Tanga, liliweka mtego na kutangaza kuinunua simu ya mkononi ya msanii huyo aina ya 

‘blackberry’ ndipo moja kati ya wanaodaiwa vibaka waliohusika kwenye tukio hilo, alipojitokeza na kuipeleka kwa ajili ya kuiuza.

Kwani walipofika eneo ambalo walikubaliana, walikabidhi simu hiyo kwa ajili ya kuikagua, lakini baadaye wezi hao walishtukia mtego huo na kukimbia huku
 wakiiacha simu hiyo.

Aidha, Kamanda Massawe alivitaja vitu ambavyo vimesalimishwa kwa jeshi hilo 

kuwa ni simu ya mkononi aina ya blackberry, Betri la gari, tairi la akiba, radio 

ya gari, begi ambalo lilikuwa na nguo za marehemu, saa ya mkononi na nguo 

ambazo alikuwa amevuliwa na vibaka wa eneo hilo mara baada ya kutokea ajali hiyo.

Mpaka kufikia sasa, msako unaendelea na wamebaini baadhi ya washukiwa wa 

uhalifu huo wamezikimbia nyumba zao kwa hofu ya kukamatwa.

Polisi wako kwenye uchunguzi mkali ili kuhakikisha wanawatia mbaroni wale 

wote ambao waliohusika na kitendo cha kinyama, alichofanyiwa msanii huyo.



Tuesday, November 27, 2012

SHARO MILIONEA AFARIKI DUNIA KWA AJALI YA GARI



MSANII WA VICHEKESHO NA MUZKI SHARO

 

MILIONEA  AMEFARIKI LEO HUKO MUHEZA

 

TANGA KWA AJALI YA GARI AMBAPO NDUGU


 YAKE WA KARIBU SNURA MUSHI 


AMETHIBITISHA  TUKIO HILO  KWA NJIA YA 


SIMU .....

 

Naye Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Afande Constatine Masawe, amethibitisha  kutokea kwa  kifo cha  wa Sharobaro, kufuatia  ajali ya gari  katika kijiji cha Lusanga, Muheza, mkoani Tanga  ambako ndio nyumbani kwao.......

 

MPAKA SASA MWILI UPO  HOSPITALI TEULE   YA MUHEZA ,TANGA


kikwatojr.blogspot.com imepokea habari hizi kwa mstuko na masikitiko makubwa kwani nyota ya Sharo Milionea ndiyo ilikuwa inaanza kung'ara katika anga za muziki pamoja na matangazo ya biashara, akiwa kayapumulia pumzi mpya wa ubunifu na weledi katika kupeleka ujumbe kwa watazamaji ambao wakubwa na wadogo walimpenda.

Tunaamini katika tasini ya filam na vichekesho kutakuwa na pengo kubwa sana kwani alikuwa ni mchekeshaji marufu sana na hata katika tasnia ya bongo freva pia kutakuwa na aliweza kufanya kazi kubwa na nzuri na wasanii wa hapa nchini pamoja na wasanii wa nnje na nyimbo yake ya mwisho inafahamika kama kizunguzungu akiwa amemshirikisha msanii alikiba na inafanya vizuri kwa sasa .

   Wote kwa pamoja na blog hii ina wapapole mashabiki na wapenzi wote wa Sharo milionea Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi amen.

Thursday, November 22, 2012

IMEELEZWA YAKUWA LAPTOP KUPUNGUZA NGUVU ZA KIUME NA NA KUHARIBU MBEGU ZA UZAZI

Imedhibitiswa kitalamu kwamba joto linalo tolewa na lap top inapotumika ikiwa mapajani hupelekea kuhalibika kwa mbegu za kiume na kuwafanya wanaume kushindwa kupata watoto kwa wapenzi wao pindi tuu wanapo hitaji kufanya hivyo na kupelekea kutafuta machawi ni nani katika familia.

Scott Reed alifikiria kwenda na mkewe hospitali kujaribu njia ya kupandikiza mimba baada ya kuhangaika muda mrefu kujaribu kupata mtoto bila mafanikio.

Kitu ambacho Scott hakuweza kukifikiria ni pale alipoambiwa na madaktari kuwa laptop yake anayoitumia mara kwa mara akiwa ameiweka mapajani ndio chanzo cha tatizo lake la kutopata mtoto.

Madaktari walimuambia kuwa joto linalotokana na laptop yake inapotumika ikiwa mapajani husababisha kuharibika kwa mbegu za kiume na hivyo kumfanya ashindwe kupata mtoto.

Scott mwenye umri wa miaka 30 aliamua kuanza kuitumia laptop yake akiwa ameiweka kwenye meza na matunda yake yalijionyesha baada ya miezi mitatu ambapo mkewe Laura ambaye naye ana umri wa miaka 30 alipopata ujauzito.

Hivi sasa ikiwa ni miezi 10 baada ya kuzaliwa kwa mtoto wao wa kike Taryn, Scott na mkewe ambao wanaishi kwenye mji wa Clanfield, Hants, bado hawaamini jibu la tatizo lao kuwa lilikuwa ni laptop.

"Sikuwahi kusikia kuhusiana na laptop kuharibu mbegu za kiume, nilishtuka sana", alisema Laura.

"Scott alikuwa akiitumia laptop yake kila siku jioni kwa masaa kadhaa akiwa ameiweka mapajani huku tukiangalia TV, hatukuwahi kufikiria kuwa ilikuwa na madhara na ilikuwa ikiharibu mbegu zake za kiume", aliongeza Laura.

Naye daktari bingwa wa masuala ya uzazi Sue Kenworthy alithibitisha madhara ya laptop kwa kusema kuwa wanaume inabidi watumie laptop wakiwa wameiweka kwenye meza badala ya kuiweka mapajani.

UAMSHO SASA WAPUNGUZIWA UNAFUU WA KUWEZA KUPATA ZAMANA


Kutokana kwa kushindwa kuhimili ma shariti ya zamana yaliyo tolewa awali na mahakama ya Mwana kwereke iliyopo visiwani Zanzibara Mahakama hiyo imependekeza kupunguza kwa viongozi hao wa jumuiya ya uamsho zanzibar

Hiyo imetokana na watumishi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kushindwa kujitokeza kuwadhamini washitakiwa hao

Awali washitakiwa hao walitakiwa kuwasilisha wadhamini wawili wanaofanya kazi serikalini ikiwa na kusaini hati ya milioni moja kila mmoja sharti ambalo limeonekana kuwa kikwazo kwao

Hivyo Hakimu Msaraka Ame Pinja alikubali kupunguza masharti hayo kutokan na wakili wa upande wa utetezi, Salum Tawfq kuomba kupunguzwa na kuangaliwa upya masharti ya dhamana kwa wateja wake

Hivyo walitakiwa kila mshitakiwa kusaini dhamana ya fedha taslimu Sh. 500,000 za kitanzania na awe na wadhamini wawili na kupunguza mmoja ambao pia ni lazima wawe watumishi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Mh Sugu, Fid Q ndani ya BONGO MOVIE!


Mheshimiwa Mbunge wa jimbo la Mbeya  mjini Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ameshiriki katika filamu inayoitwa Bifu akiwa pamoja na mwanahiphop mwenzake Fid Q.

Filamu  hiyo inaelezea maisha ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya wakiongelea maisha yao pamoja na changamoto wanazokutana nazo kila siku.

Ukiachilia mbali wasanii kama  Fid Q na Sugu yupo pia mwanadada muigizaji wa siku nyingi Christina John maarufu kwa jina la Sintah.

Thursday, November 15, 2012

green-world-health kuwatibu wakazi wa jiji la tanga matatizo mbali mbali

watalamu wa kutoa huduma ya tiba mbadala kwa kutumia virutubisho  marufu kama dawa liche huduma hizo ambazo hupatikana jijini Arusha na Dodoma amapo kwa sasa wako jijini tanga kwa jijini Arusha  wanafahamika kama ARUSHA THERAPEUTIC CLINIC ambapo wapo SAFARI HOTEL BUILDING  gorofa ya 2 chumba namba 203 kwa Dododma wanafahamika kwama THE GREEN HOUSE OF HEALTH wanapatikana Area C karibu na SIMBA HOTEL .
   kwa mawasilianao waweza kuwasiliana nao watalamu hao wa afya uweze kupatiwa tiba lishe kitaalamu kwa simu no 0717 2226566 ama 0767 226566

picha ni aina ya dawa mbali mbali ambazo hutumika kutibu maradhi mbali mbali yatokanayo na lishe ambayotunazo kula na dawa hizo hazina kemikali kwani hutokana na matunda na mboga mbago na michanaganyiko mbali mbali.
wakiwa ziarani jijini tanga wakiwapatia huduma ya tiba wakazi wa jiji la Eanga picha ni moja kati ya wateja ambao blog ya kikwatojr.blogspot.com iliwashuhudia wakipatia tiba kwa kutumia vifaa vya kisayansi zaidi.
picha ni mashine inayotumika kufanyia uchunguzi wa magonjwa mbali mbali yaliyopo katika mwili wa mwanadam inayo julikana kwa jina la kitalam QUANTUM

Pichani ni ndoo ya maji meupe kabisa yakiwa na kifaa kinacho tumika kitolea sumu mwilini kabla ya mgonjwa haja dumbukiza miguu humo ndani.
moja kati ya wateja waliohudhuria katika matibabu hayo akiwa ametumbukiza miguu ndani ya ndoo ya majii kwajili ya kutolewa sumu mwilini kwa kutumia mashine malum.
 picha hii inaonesha jinsi maji yalivyoo badilika kutoka kwenye weupe hadikuwa na rangi hiyoo unayo  jionesha hapo na hiyo ni sumu zilizopo mwilini ambao hutokana ma mavyakula tunayokula na matatizo mengine ya kibina damu.
 KWA MAWASILIANA ZAIDI WAWEZA WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0717 2226566 ama 0767 226566

Tuesday, November 13, 2012

GREEN WORLD HEALTH

Watalamu wa Tiba mbadala kwa matatizo ya kiafya yanayo sababishwa na  maisha ya kila siku pamoja  na lishe tunayo sasa   kuwasili jijini tanga kwajili ya kukupatia ufumbuzi wa matatizo yako yanayo kusumbua .

BLOG YA KIKWATOJR.BLOGSPOT.COM ITAENDELEA KUKUPA TARIFA ZAIDI JUU YA WAPI KWA KUWAPATA NA KAZI ZAO WANZO ZIFANYA KWA SASA WAKIWA JIJINI TANGA

Sunday, November 11, 2012

KUTAMBIANA KWA WASHABIKI WA COAST UNION NA YANGA

Yanga leo hawatoki...! Shabiki maarufu wa klabu ya Coastal Union, Ibrahim 'Ibra' akionekana katika Barabara ya 8 jijini Tanga mchana huu baada ya kukamilisha michoro yake mwilini akiwachiomba mkwara Yanga kabla ya kwenda uwanjani kuishangilia timu yake itakayocheza jioni ya leo dhidi ya Yanga kukamilisha mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga leo Novemba 11, 2012. 

Mashabiki wa Yanga wakiandamana na vigoma na vuvuzela katikam maeneo ya stendi kuu ya mabasi jijini Tanga leo ikiwa ni mikwara yao kabla ya kuwavaa Coastal Union kwenye Uwanja wa Mkwakwani jioni.

Mechi kali ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara itakayokuwa ya kumalizia mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo kati ya wenyeji Coastal Union na Yanga kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga leo jioni imeandika rekodi baad ya tiketi zake kuuzwa kwa bei 'mbaya' kuliko mechi zote za msimu huu ikiwamo ya mabingwa watetezi, Simba dhidi ya wenyeji hao (Coastal).

Mauzo ya tiketi hizo leo ni Sh. 5,000 kwa kiingilio cha chini (ambazo kufikia saa 9:00 watu walikuwa wakizilangua kwa Sh. 7,000), Sh. 10,000 na Sh. 15,000 kwa kiingilio cha juu wakati katika mechi nyingine zenye mvuto zaidi ikiwamo ya Simba dhidi ya Coastal, viingilio vilikuwa Sh. 4,000, Sh. 7,000 na Sh. 10,000.

Licha ya viingilio hivyo vikubwa, mashabiki walionekana wakichangamkia tiketi hizo kwa wingi, wengine wakitokea jijini Dar es Salaam na baadhi katika maeneo ya jirani ya jiji la Tanga kama Kabuku, Mwakidila, Duga Maforoni, Pangani, Muheza, Korogwe na kwingineko


Saturday, November 10, 2012

mdau kuchukua gamba lake la levo ya diploma ya jounalism Arusha hongera sana

mdau wa blog ya kikwatojr.blogspot.com Beatrice  ishengoma akiwa katika tabasamu safiii
hapa wakiwa katika bozi la kupata pichaBeatrice  ishengoma pamoja na mdau Hepy msemwa baada ya kupada diploma yao ya maswala ya uandishi wa habari na utangazaji.
hawa nao ni miongoni mwa wahitimu wa jounalism katika cho cha Arusha Jounalism Training Collage kilichopo jijini arusha maeneo ya mbauda kwamrombo.
Mdau huyu bwana Amani James akiwa katika masikitiko makubwa baada ya wezake kuweza kumaliza katika chuo hicho nae anachukua levo ya diploma ya jounalizm . blog ya kikwatojr.blogspot.com inawatakia mafanikio mema katika kazi zao za mikono.

Thursday, November 8, 2012

tarime sasa kwaendelea kuchafuka







ARIME.habari na mwandi wa blog kutoka tarime Ahmad nandonde


SERIKALI imetakiwa kuingilia kati mgogoro wa ardhi baina ya wananchi wa mtaa wa Msati kata ya Nyamisangura na Jeshi la wananchi JWTZ Nyandoto Wilayani Tarime ili kuepuka athari zinazojitokeza na kwamba endapo mgogogro huo usipotatuliwa unaweza kuvunja mahusiano mazuri kati ya Wanajeshi na wananchi.



Akiongea na waandishi wa habari  Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ambaye pia ni Diwani wa kata ya Sirari Amos Sagara ( CCM) alisema kuwa  Novemba 7 majira ya alfajiri baadhi ya mashamba ya viongozi wa Chadema na wananchi wengine yanadaiwa   kufekwa na wananjeshi wa JWTZ Nyandoto kwa mujibu wa maelezo ya wananchi.



Sagara alisema kuwa kwa sasa wanafatilia  ili kupata ukweli wa watu waliohusika kuharibu na kufeka mazao ambapo pia alisema kitendo cha kufeka mazao ni kukaribisha njaa kwa wananchi hasa waliofekewa mazao ambapo alilaani kitendo hicho kuwa kina rudisha nyuma maendeleo.



Aliongeza kuwa kwa maelezo ya wananchi  wanadai  kuwa chanzo cha mazao  yao kufekwa kinatokana na mgogoro wa ardhi na mipaka kati ya wananchi na wanajeshi ambapo wanajeshi  wanadai kuwa wananchi wamevamia  na kuishi maeneo ya jeshi huku wananchi nao wakidai wao ndio wamiliki halali wa ardhi.



Sagara alisema kuwa endapo Serikali itatatua mgogoro huo kwa kuzingatia taratibu za sheria za ardhi itasaidia kuondoa mgogoro huo wa wanajeshi na wananchi kwani itaonyesha nani mmiliki halali wa ardhi na kwamba endapo eneo  ni lajeshi  kuna haja ya Serikali kuwatafutia maeneo wananchi maeneo mengine ya kuishi.



Mashamba yanayodaiwa kufwekwa na jeshi la JWTZ Nyandoto ni  shamba la Diwani wa kata ya Nyamisangura Thobias Ghat,Mwenyekiti wa mtaaa wa msati kata ya Nyamisangura Zacharia Ghati,mwingine ni Machango Gebeno.
Rorya.



DIWANI wa kata ya Ikoma Wilayani Rorya Mkoani Mara Laurent Adriano( CCM ) amewataka wananchi wa kijiji cha Ikoma kuachana na ukabila badala yake  wafanye maendeleo kwa madai kuwa kuna ukabila kati ya Waluo na Wakurya jambo linalorudisha nyuma maendeleo ya kijiji.



Adriano alisema  kuwa kijiji cha Ikoma kina mgogoro wa ardhi kati  ya watu wa kabila la wakurya na Wajaruo ambao chanzo chake kianatokana na kutofanyika kwa uhakiki na usajiri kwa Wakurya waliohesabiwa kuwa wana Ikoma Rorya  ili wananchi wa Ikoma wawatambuwe lakini hadi sasa haujafanyika usajiri.



Hayo aliyasema wakati wa mkutano wa wananchi wa Ikoma uliokuwa ukizungumzia usajiri wa Watu  ambao  ni Wakurya ambao walikuwa wakijihesabu kuwa ni Wana Tarime Richa yakuwa Serikali  wakati ilipotenganisha Wilaya ya Rorya na Tarime waliweka mipaka  ambapo wananchi wa kitongoji cha Nyamuhunda ambao ni wakurya walihesabiwa kuwa wana Ikoma –Rorya.

“Kuna ukabila hapa Ikoma  wakati serikali imeweka mpaka wakurya wa nyamuhunda walihesabiwa kuwa Rorya  wakaambiwa wanatakiwa kufanya maendeleo Rorya  lakini nasikitika inapofanyika mikutano ya wananchi hawahudhulii na wala hawafanyi maendeleo ya kijiji lakini mashamba wanayolima  ni ya wanaikoma ambayo walipewa na Mwenyekiti wa kijiji  na aliyekuwa Mtendaji  wa kijiji na wa kata ambao kwa sasa watendaji hao wamehamishwa”alisema Adriano.



Adriano alisema kuwa  Mkuu wa Mkoa wa Mara John Tuppa aliagiza Halmashauri ya Rorya kufanya usajiri kwa watu wa Kitongoji cha Nyamuhunda ambao walihesabiwa kuwa wanaikoma  ili waweze kufanya maendeleo Rorya nakwamba nivema sasa usajiri wa watu wa nyamuhunda  ukafanyika ili kuweza kutambuliwa na wananchi wa Ikoma na waweze kufanya maendeleo  kwa kile kilichoelezwa kuwa tayali watakuwa wanafahamika kwa wanaikoma.
Powered by Blogger.