Blogger Widgets August 2012 | Mfaume Kikwato JR

PALACE HOTEL

PALACE HOTEL

Vumbua Hazina chini ya kizibo

Vumbua Hazina chini ya kizibo
+255788788218

BAYPORT

BAYPORT
KOPA BAYPORT

Thursday, August 30, 2012

hata hivi pia vinatokana na mkongee kwanini tusijikite huko na sisis tukaanza kuanzisha kilimo cha mkonge

amakweli mkongee unathani kubwa sana hembu tizama vitu vinavyotokana na mkonge


MWANADADA RYC KIUNO BILA MFUPA AKANA SHUTUMA JUU YA UJIO WAKE WA BONGO




SIKU chache baada kukanyaga ardhi ya Bongo kutoka uhamishoni nchini Kenya, nyota wa muziki wa kizazi kipya Afrika mashariki Rehema Charamila amesema kuwa hajarejea nchini kusaka wanaume. Akizungumza juzikati jijini Dar Ray C amefunguka kuwa hakuja Tanzania kutafuta Bwana wa Kuolewa nae kama watu wanavyovumisha mitaani isipokuwa amefanya hivyo kwa ajiri ya mapumziko na kazi pia. "Unajua mimi niliamua kuhamia Kenya baada ya kuona kuwa ninsupport kubwa kwa Mashabiki wa huko kuliko hapa Tanzania hivyo nikaamua kwenda kuwapa kile wanachokipenda na pia kujaribu kukuza muziki wangu, katika kusibitisha hilo hivi karibuni natarajia kuachia ngoma yangu mpya amabayo nimeipa jina 'Moyo Waniuma' alisema Ray C amabaye kwa sasa yuko nyumbani kwao bongo dar es salam.

kichupa cha tunda maniiii hichooo demu sio

k

kichupa cha sharooo milioneaaa hichooooooo


nidanganye ya sheta akiwa na raisi wa wasafi


Wednesday, August 29, 2012


MPINI MPYA WA KAMATA MWIZI MEN ft MZEE WA SINDERELA ALI K!

Msanii huyo alisema kwamba mpaka sasa bado hawajajua jina kamili la mpini huo, kwani jina walilokuwa wamependekeza  limetumika na wasanii wengine kwenye nyimbo zao.

Alisema anasubiri wakae kikao na uongozi wake, ili wamsaidie kupendekeza jina la wimbo huo.

Anasema akipendekeza jina hilo pekeyake, inawezekana lisiwe na mvuto kwa mashabiki wake kwa sababu anaweza kusababisha kupoteza malengo yake kwenye muziki.

Naweza kuzungumzia ni yule Msanii wa vichekesho na pia ni mwanamuziki wa kizazi kipya hapa nchini, Hussein Mkieti ‘Sharo Milionea’ anajipanga kuachia wimbo wake mpya ambao amefanya na mkali wa bongo fleva nchini, Alikiba.

Kwani mbali na hilo aliwaomba mashabiki wake waendelee kumpa sapoti kwenye kazi na kwamba, baada ya kuachia wimbo huo, atakuwa na mchakato wa kuufanyia video ili kuwapa burudani iliyokamilika mashabiki wake.

Mbali na kuchomoka na kibao hicho, Sharo Milionea kwa sasa anatamba na kibao chake cha ‘Chuki ni Bure’ alichomshirikisha nyota wa muziki huo, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’.

agost29


  KOFI alilo mpiga dem kwenye video lamfanya Linex aombe radhi!

Siku chache baada ya msanii Linex kutoa video ya wimbo wake (AIFOLA), ametambaa na ukurasa wake wa kuuzia sura (Facebook), akiomba radhi kwa wanawake wote kutokana na kipande cha video yake ikimuonyesha akimtandika kibao demu aliyekuwa anaigiza nae katika video hiyo kutokana na kupata malalamiko mengi yanayodai kuichochea jamii katika vitendo hivyo hasa kwa wanaume.
"Naomba radhi kwa kila mwanamke Duniani kofi nililompiga video gal wa kwenye video yangu ya 'Aifola', sikua nakusudia uchochezi wa mwanamke kupigwa na mwanaume wake natumai wanaume wenzangu mmenielewa lengo ilikua kutafuta uhalisia wa matukio kwenye video yangu..mwanamke hapigwi analiwazwa na kubembelezwa..." amesema linex

Tuesday, August 28, 2012


                CHAMA CHA ADC SASA CHAKABIDHIWA USAJIRI WA KUDUMU

Baada ya kutafuta usajili kwa muda mrefu sasa chama cha ALLIANCE FOR DEMOCRATIC CHANGE ADC kimeweza kupewa usajili wa kudumu utakacho kiwezesha kuingia rasimi katika kinyanganyiro cha uraisi mwaka 2010 ilikuweza kusambaza ilani ya chama hicho sasa kimepewa mashaririki ya kuhakikisha wanakuwa na matawi katika mikoa yote ya Tanzania bara na Tanzania visiwani ilikuweza kukiruhusu chama hicho kushiriki katika uchaguzi mkuu.
Mwenyekiti wa chama cha ALLIANCE FOR DEMOCRATIC CHANGE ADC Bw.Said Miraji akiwasili katika mkutano mkuu wa chama hicho kwaajili ya kuongea wanachama wake  baada ya kukabidhiwa cheti cha kudumu na John Tendwa msajili wa vyama vya siasa Tanzania jana katika ukumbi wa Hoteli ya Lamada jijini Dar es salaam.
Mwekiti wa Chama cha ADC Bw.Said Miraji katikati akiongea na wanachama wake mara baada ya kukabidhiwa cheti cha kudumu na John Tendwa msajili wa vyama vya siasa Tanzania jana baada ya kutimiza masharti alioyoopewa. ambapo kilipatiwa usajili wa muda tarehe 26 machi 2012 (kulia) ni katibu mkuu wa chama cha (ADC) Bw Kadawi Lucas(kushoto)Mwanachama  wa chama FORD Bw.Ramadhani Mohamedi.
Wanachama wa chama hicho wakiwa katika mkutano huowao uliofanyika kwenye hoteli ya Lamada jijini Dar es salaam jana.

NIGER, GHANA MABINGWA WAPYA AIRTEL RISING STARS AFRIKA 2012


Niger wakishangilia ubingwa wa Airtel Rising Stars Afrika 2012



MASHINDANO ya Airtel Rising Stars Afrika 2012 yaliyoshirikisha mataifa 15 barani humu yamehitimisha juzi jijini hapa, ambapo mgeni rasmi wa fainali na nyota wa zamani wa ManchesterUnited, Peter Schmeichel, alikabidhi medali na zawadi kwa washindi upande wa wavulana na wasichana.

Niger walifanikiwa kutwaa ubingwa wa kwanza wa michuano ya kwa wavulana, katika fainali ya michuano hiyo, huku Ghana wakitawazwa mabingwa upande wa wasichana katika mashindano hayo – yaliyoanza na timu 18,000 na kujumuisha vijana walio chini ya miaka 17 wapatao 324,000 Afrika nzima.

Niger iliifunga Zambia kwa penati 5-4 kushinda ubingwa Airetl Rising Stars 2012 kwa wavulana, baada ya kumaliza dakika 90 bila ya kufungana licha ya kosa kosa nyingi kwa kila timu, ambapo pia dakika 30 za nyongeza pia hazikutoa mshindi na kulazimika kupigiana penati.

Mamane Karibou, Issa Souleymane, Abubacar Timbo, Idrissa Amadou na Issifou Garba wa Niger walifunga penati, kama ilivyokuwa kwa Wazambia Timothy Sakala, Thomas Juma Mutale, Dennis Chebuye na Albert Bwalya, huku Shadrack Chimanya akikosa mkwaju wake muhimu.

Katika fainali ya wasichana, Ghana walitoka nyuma na kuwafunga wenyeji Kenya waliokuwa wakipewa nafasi kubwa ya kushinda na kuwachapa mabao 2-1.

Kenya walipata bao la uongozi lililowekwa nyavuni na Vivian Odhiambo dakika ya 27, kabla ya Emelia Lokko kuisawazishia Ghana 43 na pambano kuingia mapumziko kwa sare ya bao 1-1. Ghana ikarejea kipindi cha pili ikiwa tishio zaidi, ambapo Patience Narh aliifungia bao la ushindi 56 na kuwaduwaza Wakenya.

Wachezaji vijana 432 walishiriki fainali hizi jijini Nairobi kwa wiki nzima, wakiwezeshwa katika kila mahitaji na wadhamini, waratibu na waendeshaji wa michuano hiyo kampuni ya simu za mkononi ya Airtel, huku vijana hao wakionyesha vipaji vya hali ya juu na kutoa taswira njema ya soka la Afrika.

Mabingwa Niger na Ghana walizawadiwa fedha taslimu dola za Kimarekani 10,000 kila moja, huku zikipata fursa kwa wachezaji wake wote kushiriki Kliniki Maalum itakayofanyika hapa Nairobi na Accra, Ghana, chini ya wakufunzi wa soka kutoka klabu za Arsenal na Manchester United za England.

AGost29


ANELIKA SASA KIWANGO KIKO JUU ZAIDI YA KALE?



 Nicolas Anelka akiwa katikamoja ya mechi za klabu yake ya Shanghai Shenhua ya China



SHANGHAI, China 


WASHAMBULIAJI wa zamani wa Chelsea, Didier Drogba na Nicolas Anelka wanaweza kuuzwa na Shanghai Shenhua ya China kutokana na kuongezeka kwa gharama za uendeshaji zinazoikabili klabu hiyo na kuzua mgogoro miongoni mwa wanahisa.

Mwenyekiti wa Shanghai Shenhua, Zhu Jun, ambaye ana asilimia 28.5 ya hisa, ilikuwa alipe tu sehemu ya gharama za kila siku za klabu ambapo kwa madai yake udhibiti wa mahitaji na matumizi ya siku haukuweza kudhibitiwa, gazeti la China Daily limefichua.

Makubaliano ya awali yalikuwa, kama Zhu angewekeza dola milioni 23.6 katika klabu hiyo kwa zaidi ya miaka miwili, hisa zake zitapaswa kupanda na kufikia zaidi ya asilimia 70, gazeti hilo lilifichua.

Gazeti jingine la Oriental Sports Daily liliripoti kuwa Zhu aliwekeza zaidi ya dola za Kimarekani milioni 94 katika kipindi cha miaka mitano na nusu, wakati makampuni yanayomilikwa na serikali hayakutumia chochote.

"Hali imekuwa tatanishi na jambo baya zaidi kwetu ni majukumu mazito miongioni mwetu," taarifa rasmi ya klabu ilisema na kuongeza: "Tatizo kubwa ni kwamba, uendeshaji wa masuala ya kipesa na kazi kwa klabu hayawezi kufanywa nje ya taratibu.

"Jambo hilo limezua sintofahamu na kuweka shakani mustakabali wa maendeleo na ustawi wa Shenhua."

Kama hali ya mambo haitopatiwa ufumbuzi, Zhu, ambaye ndiye anayesaini cheki zote za malipo klabuni, anaweza kuamua kuweka kwenye soko la hisa, asilimia yake 28.5 ya hisa zake, kitu ambacho kitaathiri kwa kiasi kikubwa mapato na mishahara ya wachezaji.

Hali hiyo inazua shaka matarajio ya Drogba na Anelka kuweza kubakishwa Shenhua, kutokana na mishahara mikubwa ya pauni 300,000 kwa wiki wanazolipwa kila mmoja.

Pamoja na kutumia pesa nyingi kuisajili nyota wenye majina makubwa, Shenhua iko nafasi ya 10 kati ya timu 16 zinazoshiriki Ligi Kuu ya China, ikiwa na pointi 27 ilizovuna katika mechi 23, pointi 20 nyuma ya vinara Guangzhou Evergrande yenye pointi 47.

Sunday, August 26, 2012

Agost26

                        TANGA SENSA KWAPAMAZUKA.

Zoezi la sensa ya watu na makazi limeanza rasimi usiku wa mkuamkia leo kote nchi ambapo katika mkoa wa Tanga hususani katika wilaya ya Mkinga mandalizi ya kuandaa zoezi hilo yamekwisha kamilika .


Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Mkinga bi Mboni Mgaza wakati akizungumza na wandishi wa habari mapema hii leo alisema kuwawananchi wa wilaya hiyo wako tayari kwa ajili ya kuhesabiwa kutokana na zoezi hilo kwenda sambamba na uandikishaji wa vitambulisho vya taifa.


Mkuu huyo wa wilaya ya Mkinga alisema kuwa wananchi wa wilaya hiyo hawana budi kushiriki kikamilifu kwenye zoezi hilo kwani manufaa yake ni makubwa sana hasa wakati huu taifa likiwa linaandikisha vitambulisho vya ukazi na aliwasihi viongozi mbalimbali wa dini na vyama vya siasa kuendelea kuhamasisha watu wao kuweza kushiriki kikamilifu zoezi hilo .


Huku hayo yakiendelea jeshila polisi mkoa wa Tanga nalo limetoa tamko lake kwa yeyete atakae kwamisha zoezi hili la sensa kwa kuwashawishi watu wengine wasishiriki zoezi hilo basi sheria kali itachukuliwa juu yao.


Hayo yameelezwa na kamanda wa polisi mkoa wa Tanga Costantin Masawe kuhusiana na watu ambao wanasambaza vipeperushi kwa wananchi ilikuzuiwa kuhesabiwa kwa itikadi za kidini na kuahidi kuwa hata mara baada ya zoezi hili la sensa kumalizika hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wale ambao walikuwa wakiwashawishi watu kukataa kuhesabiwa kwani kwasasa wanaendelea na uchunguzi ilikuweza kuwabaini watu hao.

Saturday, August 25, 2012


COAST UNION WAGOSI WA KAYA WAFANYA UCHAGUZI MDOGO WA CLAB HIYO

Hatimaye wagosi wa kaya timu ya COAST UNION hii leo imefanya uchaguzi uliokuwa na lengo la  kukamilisha uongozi wa timu hiyo yenye maskani yake jijini Tanga.

Katika uchaguzi huo uliofanyika kwa uwazi na huru ulikuwa na lengo la kujaza  nafasi za wajumbe wa kamati pamoja na makamu mwenyekiti ambapo katika nafasi ya wajumbe awaligombea wajumbe wawili ambao ni ndugu  TAITASI BANDAWE naDR AHMEDI TWAHA ambapo wote waliweza kuchaguliwa kwa kupata kura zaidi ya 26 kwa mujibu wa sheria za WAGOSI HAO WA KAYA.

Katika uchaguzi huo TAITASI alipata kura 41 na DR TWAHA alipata jumla ya kura 44 kati ya 49 za wajumbe wote walio huzulia katika uchaguzi huo.

Na kwa nafasi ya makamu mwenyekiti ilikuwa na mgombea mmoja ambaye ni STEAVEN MNGUTO ambaye ndiye mshindi  wa nafasi hiyo ya makamu mwenyekiti ambapo alipata jumla ya kura 46 kati kura 49 za wajumbe walio huzulia katika kikao hicho  cha uchaguzi.

Sasa wajumbe haowanatambulika kihalali na tayari kuanza majukumu yao kwa kuwa tayari ni wana coastal union. 

Kabla ya uchaguzi huo kufanyika wajumbe walipata nafasi ya kuzinadi sera zao mbele ya wajumbe ambapo wote walionekana kuwa na nia moja ya kuipeleka mbele kimafanikio timu yao kwa kusisitiza ummoja na mshikamano na kuwataka kuondoa makundi na kuweka mbele maslahi ya timu ili iweze kupata mafanikio zaidi katika soka la ndani na katika medani za kimataifa.pia wamesema kuwa wameweka malengo ya kunyakuwa ubingwa msimu huu wa ligi kuu Tanzania bara au nafasi ya pili itakayo wawezesha kucheza michuano ya kimataifa hivyo  wamewaomba wanachama pamoja na vingozi kuziondoa tofauti zao na kuukumbatia umoja wati mu.

Naye mwenyekiti wa timu hiyo ya wagosi wa kaya AHMEDI AURORA amewashukuru wajumbe wote kwa kufanya uchaguzi huo kwa uhuru na haki na amewataka wote kwa pamoja kuifanya timu hiyo ifanye vyema kwa kutimiza majukumu yao bila kusukumwa.

Timu hiyo ipo katika maandalizi ya ligi kuu na inatarajia kucheza mechi za kirafiki na timu za Mafande wa polisi Moro,KJT Oljoro ya Arusha na baadaye watacheza na timu ya BANDARI ya nchini Kenya.





MKOA WA TANGA KUTOA WIJANA KWAAJILI YA KUSHIRIKI MASHINDANO YA RIADHA TAIFA




wachezaji walioshiriki mashindano ya riadha mkoa wa Tanga ambayo yalijumuisha wilaya zote tisa za mkoa wa Tanga.


picha ni washindi walioshinda katika mashindano ya riadha mko wa Tanga kuweza kwenda kushindana kitaifa kukimbia mita mia kwa wanaume na wanawake mita 200,400na mita 1500 bila kuwasahau washindi katika kurusha mkuki na kurusha tufe kwa wanaume na wanawake

Thursday, August 23, 2012

WAKULIMA WA MKONGE KAENI MKAO WA KULA TANGA

mkonge ni zao linalo stamili magonjwa na halidhuriwi kirahisi ma wadudu hivyo sasa wakulima wa zao hilo la mkonge wameaswa kuongeza nguvu katika uzalishaji wa zao hilo kwani kwa sasa mkonge unamatumizi mengi ukiacha kutumika kutengenezea kamba.

Mkonge pia hutumika kutengenezea composite ambayo hutumika kutengenezea bidhaa mbalimbali za thamani,Mkonge kwa sasa unatumika katika katika tasinia ya magari,ndege,meli,na ujenzi wa nyumba za bei nafuu.









                                                                                                      pichani kulia ni Mkurugenzi mkuu wa bodi ya mkonge Tanzania Bwana Hamisi Mapinda akiwa na meneja wa kituo cha redio Mwambao Fm kilichopo Jijini Tanga Bwana Hashim Fadhili.

Wednesday, August 22, 2012


JESHI la polisi Tanzania limetoa ajira 1,446 kwa Vijana wa kidato cha nne wa mwaka 2011,kidato cha sita mwaka 2012 na vijana walioko kambi za JKT Mafinga, Mlale, Ruvu, Mgambo Oljoro , Bulombola, Kanembwa, Itende, Nachingwea na Mgulani.


Kati ya hao  951 ni walio hitimu kidato cha nne na sita mwaka 2011/2012 na 495 kwa Vijana waliokuwa katika Kambi za JKT za JKT Mafinga, Mlale, Ruvu, Mgambo Oljoro , Bulombola, Kanembwa, Itende, Nachingwea na Mgulani. 


Maelekezo Muhimu:-

1. Vijana wa kidato cha nne wa mwaka 2011,kidato cha sita mwaka 2012 na vijana walioko JKT Mafinga, Mlale, Ruvu, Mgambo Oljoro , Bulombola, Kanembwa, Itende, Nachingwea na Mgulani waliochaguliwa kujiunga na Jeshi la Polisi baada ya mchakato wa usaili uliokamilika hivi karibuni wanatakiwa kuripoti Chuo cha Taaluma ya Polisi Moshi kati ya tarehe 06/10/2011 na 07/10/2012 kwa ajili ya zoezi la usajili litakaloanza chuoni hapo tarehe 8.10.2012.


2. Vijana hao wanatakiwa kuripoti tarehe 05/10/2012 kwa Makamanda wa Polisi wa Mikoa kwa ajili ya kuwaandalia usafiri wa kuwapeleka Chuoni.


3. Vijana wanaotoka katika makambi ya JKT yaliyotajwa hapo juu wataripoti kwa makamanda wa Polisi wa mikoa iliyo karibu nao.


Vijana wa kidato cha nne na sita wataripoti kwa makamanda wa Polisi wa Mikoa waliojiandikisha wakati wa zoezi la usaili lililoendeshwa mwezi Julai, 2012.


4. Atakaeamua kuripoti kwa Kamanda wa Polisi ambako hakupangiwa atalazimika kujigharimia usafiri hadi Chuo cha Polisi Moshi


5. Vijana hawa wanatakiwa kufika chuoni wakiwa na mahitaji yafuatayo:

 

a) Vyeti vyao vyote vya masomo(Academic Certificates/Result slip pamoja na Leaving certificates) kidato cha Nne/Sita, Vyeti vya kuzaliwa (Original Birth certificates). Hati ya kiapo cha kuzaliwa haitakubalika.


b) Mashuka mawili rangi ya Bluu Bahari (light blue)

c) Chandarua

d) Nguo za michezo(Track suit nyeusi,Tshirt blue na Raba)

e) Pasi ya Mkaa

f) Ndoo moja.1

g) Pesa kidogo ya kujikimu.

 

6. Kwa mujibu wa kanuni za chuo ni marufuku kufika chuoni na simu ya mkononi, atakayepatikana na simu atafukuzwa chuoni hapo. Chuo kitaelekeza na kusaidia kufanya mawasiliano. 

 

7. Hakikisha jina lako liko kwenye orodha hii. Jeshi la Polisi

halitahusika na gharama zozote kwa atakaye kiuka maagizo haya.

 

MAJIMAREFU AWAKA JIMBONI KWAKE KWA KUCHAKACHULIWA NA WATENDAJI WAKE


MBUNGE wa jimbo la Korogwe vijijini  Stephen Ngonyani alimarufu majimarefu amemtaka  Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Bungu Mohamed Kalaghe kuweza  kuvitumia vifaa vya ujenzi alivyotoa kwa ajili ya ujenzi wa  kituo cha polisi katika tarafa ya Bungu.
Mh Ngonyani aliyasema hayo wakati alipotembelea kijiji hicho akiwa maeambatana na mkuu wa wilaya ya Korogwe  Mrisho Gambo kwa lengo la kukagua ujenzi wa kituo cha polisi ambacho ametoa vifaa kwajili ya ujenzi huwo.
Akizungumza katika mkutano kijijini hapo Mh majimarefu  amesema kuwa  anahitaji ushirikiano na viongozi mbalimbali katika jimbo hilo ili aweze kutatua kero na  kukamilisha ahadi alizozitoa wakati akiwa anawaomba kura mwaka 2010 .
Vifa alivyotoa mbunge huyo kabla ya ukaguzi huwo ni  pamoja na mifuko 40 ya saruji, makopo ya ya mafuta ya rangi yeneujazo wa  lita 40, nondo 20 za milimita 12 pamoja na shilingi milioni 1.5 kwa ajili ya malipo ya fundi atakayekarabati jengo hilo amabalo amelikuta likiwa halija fanyiwa kazi yeyeote, alikuta havijafanya jambo lolote.
Hata hivyo  Mkuu wa wilaya korogwe bwana  Mrisho Gamba ameliomba jeshi la polisi kuweza kuwachukulia hatua haraiwezekanavyo mtendaji wa kijiji hicho pamoja na mwenyekiti wa kijiji kwa kwakuhujumu maendeleo ya wananchi.

TANGA SASA KUPANDISHIWA BILI ZA SHILIKA LA NYUMBA NHC LAKINI WAULA UJENZI WA NYUMBA MPYA

SHIRIKA la Nyumba la Taifa jijini  Tanga NHC limewaeleza wapangaji kuwa upandishaji wa kodi  za nyumba katika shilika hilo ni kwa lengo la kukarabati na kuboresha nyumba hizo.
Akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake mapema hii leo Meneja wa Shirika la Nyumba Mkoa wa Tanga Bw. Isaya Mshamba  amesema  kuwa changamoto kubwa inayo wakabili kwa sasa ni kuwa elimisha wapangaji wao sababu zilizopelekea  kupandisha kodi hizo. 
Aidha, ameendelea kusema kuwa imekuwa ni vigumu kuweza kuwafikia wapangaji wake wote kwalengo la kuwaeleza sababu zilizopelekea kupandisha kodi hizo hivyo amewaomba wapangaji wa shilika hilo kuweza kukubaliana na hali hiyo kwalengo la kuboresha shilika.
Hata hivyo, Bw. Mshamba ameendelea kusema kuwa mikakati waliyo nayo ni kujenga nyumba nyingine za bei nafuu na kuwauzia wananchi wote hivyo amewataka wakazi wa jijilatanga kuweza kushirikiana nao kwa pamoja.
Sambamba na hayo ameeleza kuwa  Shirika la Nyumba la Taifa NHC kwa Mkoa wa Tanga lina mpango wa kuanza zoezi lo la kujenga nyumba hizo mpya katika wilaya mbalimbali za mkoa wa Tanga na kwakuanzia na wilaya ya Mkinga.

AMAKWELI MKOA WA TANGA UMEBARIKIWA HAYA NI MANZARI YA WILAYA YA MKINGA


BADHI YA VIJANA WALIO HUDHURIA MAFUNZO HAYO WAKIPATA PICHA YA PAMOJA


HAPA MAMA AKISISITIZA JAMBO HUKU MDAU WA HABARI BWANA HASHIMU AKINUKUU KWA MAKINI

bwana hashimu fadhili akiwa anajaribu kuandika vitu vya umuhimu ambavyo mkuu wa wilaya alikuwa akivizungumza kwa makini ana hapa mkuu wa wilaya alikuwa akiwahusia vijana wa kike kujiendeleza zaidi kimasomo na kuepuka visha wishi

MKUU WA WILAYA YA MKINGA BI MBONI MGAZA AKIWA NA MDAU MKUBWA WA HABARI JIJINI TANGA

kulia ni bi mboni mgaza akiwa na bwana Hashimu Fadhili miongoni mwa wadau wakubwa wa habari katika mkoa wa tanga wakipata picha ya pamoja

MIONGONI WA DADA WALIKUWA WAKIWASILISHA MADA KWA KINADADA WENZAO

mwenyenguo nyekundu ni dada pepe akiwa na muwasilisha mada mwenzake

VIJANA WA KIKE KATIKA WILAYA YA MKINGA WAPATIWA SEMINA JUU YA MASWALA YA MIMBA ZA UTOTONI NA KUASWA KUJIKITA KATIKA ELIMU

pichani  ni mkuu wa wilaya mpya ya mkinga bi mboni Mgaza akiwa anasisitiza jambo katika semina hiyo)

Tuesday, August 21, 2012


Hatimaye Mali yaunda serikali mpya

Hatimaye Mali yaunda serikali mpya

Mali imetangaza serikali mpya, karibu miezi mitano tangu yalipotokea mapinduzi ya kijeshi yaliyomng'oa madarakani Rais Amadou Toumani Toure.

 Rais wa serikali ya mpito ya nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika, Dioncounda Traore, jana alitangaza serikali mpya yenye mawaziri 31 wakiwemo mawaziri watano ambao ni wafuasi wa karibu na kiongozi wa mapinduzi ya kijeshi, Kepteni Amadou Haya Sanogo. 

Tarehe 22 Machi mwaka huu, maafisa walioasi jeshini wakiongozwa na Kepteni Sanogo walimpindua Rais Toure na kuchukua madaraka ya nchi hiyo kwa madai kuwa Toure ameshindwa kukabiliana na waasi wa kaskazini mwa nchi hiyo. 

Hata hivyo wanajeshi hao hawakufanya chochote cha maana cha kukabiliana na waasi kiasi kwamba waasi hao walitumia fursa hiyo kuteka maeneo zaidi ya kaskazini mwa nchi hiyo na kutangaza uhuru wa eneo la Azawad.

 Ingawa Kepteni Sanogo amekabidhi rasmi madaraka kwa serikali ya mpito ya wananchi huko Mali, lakini bado anadhibiti mambo kwa nyuma ya pazia.




Kuapishwa bunge la Somalia kwamalizika salam

Kuapishwa bunge la Somalia kwamalizika salama

Zoezi la kuliapisha bunge jipya la Somalia lilimalizika salama jana Jumatatu ikiwa ni mara ya kwanza tangu alipopinduliwa dikteta Siad Bare, zaidi ya miaka 20 iliyopita huku nchi hiyo ya Pembe ya Afrika ikiendelea na juhudi zake za kumaliza mgogoro wa ndani uliodumu kwa zaidi ya miongo miwili. 

Wabunge 250 wa Somalia walikula viapo vyao jana Jumatatu mbele ya Jaji Mkuu wakiwa wameshika nakala za Qur'ani Tukufu. 

Sherehe hizo zimefanyika chini ya ulinzi mkali wa askari wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika. Nafasi ya serikali ya mpito ya Somalia itachukuliwa na bunge dogo lenye wajumbe 257 na bunge kubwa litakalokuwa na wajumbe wasiozidi 54 ambalo litachaguliwa baadaye chini ya mpango unaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa.

 Mbunge mmoja mpya wa bunge la Somalia, Siyad Shire Mahmoud amenukuliwa akisema kuwa, wabunge wapya wa Somalia wamefurahi sana kuona kuwa wamekula viapo vyao wakiwa ndani ya nchi yao. 

Jana pia bunge la Somalia liliakhirisha uchaguzi wa rais kwa muda usiojulikana kutokana na kusuasua zoezi la kuwaapisha wabunge wapya pamoja na uchaguzi wa spika.


TETESI ZA MAJUU KUHUSU UHAMISHO

Vijana wa  Liverpool wamemueleza  Andy Carroll, 23, kuamua mustakabali wake wa baadae mwishoni mwa week......

Daniele De Rossi, 29,ambaye anawindwa na Manchester city  is set to stay with Roma na kiungo  huyo ameitisha kikao leo jumanne na wahandishi wa habari kwaajili ya kutoa uwamuzi 
huwenda kiungo Tom Huddlestone, 25, akaondoka kwa mkopo White Hart Lane baada ya Stoke kuonyesha nia ya kutaka kumsajili.

na kwaupande Tottenham haina nia ya kumsajili mshambuliaji wa  Arsenal 28-year-old Marouane Chamakh.

 huku nako klabu ya Fulham ipo kwenyemazungumzo na Striker wa zamani wa Arsenal Eduardo 29-year-old  wa kitita cha £7 m kuja kuwa mbadala wa forward wa kimataifa wa marekani Dempsey ambae mapema wiki hii alikataa kuichezea timu hiyo.

BUTTENER SASA KUTUA OLD TRAFFOD KWA VIPIMO!

LEO Alexander Buttner amesafiri kutoka Schipol Airport huko Amsterdam kwenda Manchester ili kupima afya yake na kukamilisha Uhamisho wake kutoka Klabu ya Vitesse Arnhem ya Holland kwenda Manchester United.

Buttner, Miaka 23, ni Fulbeki wa kushoto ambae hivi karibuni amekuwa akiwindwa na Southampton, Fulham na Queens Park Rangers.

Akisimulia Uhamisho wake huu ambao utagharimu Euro Milioni 5, Buttner amesema: “Kama Wiki moja iliopita ungeniambia ntakuwa nikicheza pamoja na Robin van Persie ndani ya Manchester United, ningekupeleka moja kwa moja Hospitali ya Wenda wazimu!”

Aliongeza: “Mwezi mmoja uliopita, Manchester United ilituma Barua pepe ikionyesha nia yao kunichukua lakini katika Siku 4 zilizopita mambo yalikamilika. Sijaongea na Sir Alex Ferguson lakini mambo yakienda sawa itatokea tu.”

Buttner amekuwa na mgogoro na Klabu yake Vitesse Arnhem kuhusu hatima yake ya baadae na alikuwa amezuiwa kufanya mazoezi na Timu ya Kwanza huku suala lake likiwa mbele ya Vyombo vya Usuluhisho na mwenyewe amesema: “Kwa kuzuiwa kucheza na Timu ya Kwanza na Kesi yangu dhidi ya Vitesse Arnhem ikiwa kwenye Vyombo vya Sheria, Uhamisho huu ni zawadi nzuri kwangu!”

Manchester United wamekuwa wakisaka Fulbeki wa kushoto ili kumsaidia Patrice Evra kwenye nafasi hiyo baada ya mbadala wake, Fabio da Silva, kupelekwa QPR kwa mkopo.


KWA MASHABIKI WA LIGI KUU YA  UJERUMANI KUANZA IJUMAA

Mabingwa Borussia Dortmund na Werder Bremen watafungua msimu wa 50 wa ligi kuu ya Ujerumani Bundeslifa Ijumaa (24.08.20012), ikiwa ni miaka 49 baada ya timu hizo mbili kukutana katika siku hiyo ya Agosti 24 mwaka 1963.
Timo Konietzka alifunga bao la kwanza la ligi hiyo mpya lakini hakuna ushahidi wowote wa picha za gazeti wala televisheni za kuonyesha bao hilo lililofungwa katika dakika ya kwanza.

mechi ya Ijumaa hii, itarushwa moja kwa moja kwenye televisheni za ujeruman, pamoja na kompyuta, vifaa kama vile simu. 

Ligi ya Bundesliga imekuwa ni taasisi ya kitaifa ikiwa na rekodi ya wastani ulimwenguni ya uhudhuriaji wa mashabiki tangu ilipoanza kwa mwendo wa pole, kuponea sakata za kupanga mechi katika mika ya sabini na kuwatengeneza mashujaa kama vile Franz Beckenbauer, Gerd Mueller, Wolfgang Overath na Guenther Netzer.
Msimu wa kwanza wa Ligi ulikuwa na timu 16 kabla ya ligi kukua hadi tmu 18 na kwa kipindi kifupi timu 20 katika miaka ya mapema ya tisini ili kuzijumuisha timu za Mashariki ya Ujerumani baada ya muungano wa nchi hiyo. 

Bayern ambayo ilijiunga na ligi hiyo katika mwaka wa 1965, ndiyo iliyoshinda mataji 21 ikilinganishwa na matano kila mmoja ya mahasimu wake wa karibu Borussia Dortmund na Borussia Moenchengladbach.

Timu ya Now Camp leo imefanikiwa kuibuka mabingwa katika bonanza LA KUGOMBEA MBUZI lililofanyika katika uwanja wa ndani shule ya sec.Galanosi baada ya kuichabanga  Mikoroshini 1-0.

katika mchezo huo wa wafainali uliopigwa majira ya saa  11 za jioni, goli la mabingwa likifungwa na FRED DASTAN kunako dk ya 15 kipindi cha kwanza..

mpaka dk 90 zina malizika Now Camp 1-0 Mikoroshini.

Katika mchezo wa awali wa kutafuta mshindi wa tatu,Timu ya LEVOLOSTI iliibuka na ushindi mbele ya KIRARE kwa pen.4-2 baada ya kumaliza sare ya bila kufungana.

Awali bonanza hilo lilishirikisha timu 6 nazo ni ,SHASHAA,MKOROSHINI,NOW CAMP,LEVOLOST,KIRARE NA BUCHER zote kutoka Nguvumali.

mgeni rasmi alikuwa ni Mjumbe wa kamati ya utendaji wa TFF Taifa  Khaleed Abdallah,akiwa ameambatana na mmoja wa waandaaji na mwenyekiti wa vasco dagama BERNAD GORIAMA.
katika bonanza hilo  Mshindi wa kwanza ameibuka na mbuzi Dume,mshindi wa pili kreti mbili za soda na mshindi wa tatu kreti moja ya soda.

EABL yatoa Dola 400,000 kwa CHALENJI CUP 2012

Kampuni ya Bia ya East African Breweries Limited (EABL) imeahidi kutoa Dola za Kimarekani 400,000 kwa ajili ya kuendesha Mashindano ya Mataifa ya Afrika Mashariki na ya Kati, CHALENJI CUP 2012, yatakayochezwa huko Kampala, Uganda kuanzia Novemba 27 hadi Desemba 12.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye, Fedha hizo ni za udhamini ambao utalipia gharama za usafiri, malazi na Zawadi kwa Washindi zikiwa ni Dola 30,000 kwa Bingwa, Dola 20,000 kwa Mshindi wa Pili na Dola 10,000 kwa Timu ya Tatu.

Wakati huo huo, CECAFA imekubaliana na Waongoza Kampeni dhidi ya Malaria, United Against Malaria (UAM), kushirikiana na kuongeza nguvu kukabiliana na Ugonjwa huo wakati wa michuano ya CHALENJI CUP 2012.

Akizungumzia makubaliano hayo, Rais wa CECAFA, Leodegar Tenga, ambae aliisifia UAM katika kampeni yake ya kujaribu kuuondoa Ugonjwa wa Malaria ifikapo 2015 kama ilivyopangwa na Umoja wa Mataifa, amesema: “Mafanikio yetu kwenye Soka yanaathiriwa sana na Malaria hasa kwetu, Familia zetu na Rafiki zetu. Lazima tuelimishe Jamii hatari za Malaria.”

Kwenye CHALENJI CUP 2012, Sudan ya Kusini, Mwanachama mpya wa CECAFA, wanatarajiwa kushiriki kwa mara ya kwanza na hii ni mara ya pili kwa Nchi hiyo mpya kucheza Mashindano ya CECAFA, mara ya kwanza ilikuwa kwenye Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki ya Kati, KAGAME CUP, yaliyochezwa Dar es Salaam Mwezi Julai na Nchi hiyo kuwakilishwa na Wau El Saalam ambapo Yanga walitwaa Ubingwa kwa mara ya pili mfululizo.


Sunday, August 19, 2012


  USAJILI WA OCHIENG SIMBA WA GUBIKWA NA MAGUMASHI


MATARAJIO ya Wekundu wa Msimbazi kupata huduma za beki wa zamani timu ya taifa ya Kenya‘Harambee Stars,’ Pascal Ochieng, yako shakani baada ya klabu ya AFC Leopards kudai ni mchezaji wao halali. 

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation la nchini humo, Katibu Mkuu wa Leopards, ambayo ni klabu ya zamani ya Ochieng, Winstone Kitui, amesema klabu yake imesikitishwa kusikia kuwa nyota huyo amesaini mkataba wa miaka miwili Simba. 

Aliongeza kuwa, wameshitushwa kusikia usajili huo wa mabingwa wa Tanzania Simba kwa beki wao huyo, aliyejifunga kwa mkataba mfupi wa kuichezea klabu hiyo ya Ligi Kuu kwa miezi sita, kuanzia Juni mwaka huu. 

“Ochieng analijua hilo zaidi,” Kitui alisema na kuongeza: “Yeye ni mchezaji tuliye na mkataba ambaye amejiweka pabaya mwenyewe kwa kufanya udanganyifu. Nilikubali ombi la kumsajili wakati akiwa hana timu na kumpa nafasi ya kujiunga nasi.” 

Mkali huyo akajiunga Leopards akitokea Rangers FC kwa mkataba usio na malipo, ambapo Ochieng akakacha mazoezi ya klabu kwa wiki mbili, kabla ya kusikia ameamua kuachana na klabu hiyo. 

Ochieng mshindi wa Tuzo ya Beki Bora wa Mwaka wa Ligi Kuu ya Kenyamsimu uliopita, alijikuta akikosa utulivu dimbani tangu alipotimka Rangers, huku akifanya vibaya majaribio yake na klabu ya Pretoria University

Mholanzi aliyekuwa tatbibu wa Leopards, Jan Koops naye amepigwa butwaa na kusema: “Alitoweka na kuachana nasi bila mawasiliano yoyote, jambo ambalo hatukulitarajia kufanywa na yeye. 

“Simba pia ikafanya usajili wake bila kuzungumza na yeyote miongoni mwa maofisa wa klabu; badala yake, hapakuwa na taratibu zozote za kiafya kwa vipimo safi kwa mchezaji?” alihoji Koops. 

Kwa mujibu wa Daily Nation, akizungumza bila kufichua jina la kiongozi, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hanspope ametetea uhamisho wa nyota huyo na kusema ulipata baraka za Leopards, kabla ya kumsajili na kumtambulisha rasmi.


 JAMANI KUENI MACHO UTAPELI WA KUTUMIA SIMU WAINGI BAADHI YA VIONGOZI WALIZWA


Viongozi watatu wa ngazi ya juu wa Serikali ya Mkoa wa Katavi wametapeliwa na watu wasiojulikana baada ya kuelezwa kuwa wameshinda promosheni ya Airtel ya Shilingi milioni 50.


Waliotapeliwa ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt. Rajabu Rutengwe, Katibu Tawala wa Mkoa, Emmanuel Kalobelo na Mganga Mkuu wa Mkoa, Yahaya Hussein.


Viongozi hao walitapeliwa kwa nyakati tofauti na watu waliojitambulisha kwao kwa simu kuwa ni watumishi wa Kampuni ya Simu ya Airtel.


Tukio la kwanza lilikuwa ni la Mkuu wa Mkoa kuambiwa ameshinda zawadi ya Sh. milioni 50 na aliombwa awatumie namba za simu za watu watano aliozungumza nao mara ya mwisho na baada ya kufanya hivyo simu yake ya mkononi ikafungwa na matapeli hao.


Akieleza mkasa huo, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt. Yahaya alisema yeye baada ya kupigiwa simu na matapeli hao hakuwa na shaka nao kutokana na kauli yao ilivyokuwa ya ustaarabu. Alisema baada ya kuwapa majina ya watu watano alizungumza nao mara ya mwisho kwenye simu yake na kuombwa awatajie namba zake za siri za akaunti ya Benki ya NMB ili wamtumie zawadi ya Sh. milioni 50. Baada ya kuombwa namba yake ya siri, Dkt. Yahaya hakuwa na shaka yoyote na hivyo akawapatia namba hiyo ya siri. Hata hivyo hakuweza kuibiwa fedha zozote kwa vile akaunti yake haikuwa na salio la kutosha.


Meneja wa Wawi la NMB Wilaya ya Mpanda, Erick Luhanda alisema amepokea malalamiko kutoka kwa viongozi hao. Alisema kiongozi wa mwisho kumpa taarifa alikuwa ni Katibu Tawala wa Mkoa, Kalobelo. Luanda alisema tayari taratibu za kibenki zimefanyika hivyo hakutakuwa na hujuma kwenye akaunti za viongozi hao.


Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alithibitisha kutokea matukio hayo.


UNAWEZAZ KUICHEKI HAPA NGOMA MPYA YA MWANA DADA TAZM-NGOMA INAITWA KWASA KWASA


IDI KUTAWAKA MOTO NA BABA WA MUZIKII


                    Msondo, Sikinde kutafuta wa zaidi leo hii?



Mashabiki wa bendi pinzani za Msondo Ngoma na  Mlimani Park Orchestra (Wana Sikinde Ngoma ya Ukae) leo mchana watafurikia kwenye  viwanja vya Leaders Club, Kinondonikushuhudia bendi gani itaibuka 


ya leo imeandaliwa Keen Arts na kudhaminiwa na Konyagi kwa ajili ya kukusherekea Sikuku ya Iddi.

Takribani mwezi moja iliyopiata bendi hizo zilikuwa zikijiandaa na pambano ya leo ambao itamua ni bendi gain itaibuka mshindi 2012.

Mratibu wa mchuano huo Joseph Kapinga amesema pambano ya leo litakuwa la aina yake ukizingatia kuwa bendi zote zimekamilika.

Kapinga alisema ili kuondoa malamiko ya kuhujumiwa, kila bendi itatumia jukwaa lake. “Litakuwa pamabano la aina yake ukizingatia kuwa itakuwa ni mara ya kwanza kwa bendi hizi pinzani kupambana siku ya sikukuu ya Iddi tangu zianzishwe,” alisema Kapinga.Pia itakuwa ni mara ya kwanza kwao kushindana katika viwanja vya Leaders Club.

Kapinga alisema mchuano huo itaanza saa nane mchana hadi liamba.Msondo itaingia jukwaani ikitokea Dodoma ilikokuwa imeweka kambi, huku Sikinde ikitokea mafichoni.Sikinde itakuwa ikiwategemea wanamuziki wake ambao wamewasili hivi karibuni wakitokea nchini Marekani ambao ni Hassan Rehani Bitchuka na Ally Jamwaka. 

Wengine ni Hassan Kunyata, Abdallah Hemba, Habib Jeff, Yusuph Benald na wengineo wengi.Msondo itakuwa itatawakilishwa na Muhidini Maalim Gurumo, Said Mabera, Hassan Moshi, Shaaban Dede, Eddo Sanga, Abdul Ridhiwani na wengineo.

Mwaka jana bendi hizo zilipambana vikali kwenye ukumbi wa TCC Club sikukuu ya Krismasi ambapo mbali na muziki safi na vituko vya hapa pale zilitoka sare.Mratibu huyo amesema kuwa mwaka huu mshindi ni lazima apatikane hata kwa kurusha shilingi.

SIMBA WANGARA SUPAR8


Hatimaye  kikosi cha pili cha mabingwa wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara Simba ya jijini kimefanikiwa kutwaa taji la michuano ya BankABC Sup8R 2012 baada ya kuichapa Mtibwa Sugar ya Morogoro kwa mabao 4-3 mchezo uliofanyika katika uwanja wa Taifa jijini  Dar es Salaam.

Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika timu hizo zilikuwa zimefungana mabao 3-3 huku mabao ya Simba yakiwa yamewekwa nyavuni na Christopher Edward mawili na Haroun Athumani na kwa upande wa Mtibwa mabao yao yakifungwa Shabani Kisiga mabao mawili na Hasan Seif.

 Bao muhimu kwa Simba ambalo limewapa ubingwa limewekwa kimiani na Edward Christopher ndani ya dakika 30 za  muda wa nyongeza.

Mfungaji bora wa michuano hiyo amekuwa ni Edward Christopher aliyefunga mabao 9 na amepewa tuzo ya ufungaji bora.

atu peke yake na kufikisha jumla ya mabao tisa, hivyo kujinyakulia tuzo ya ufungaji bora wa michuano hiyo na kuzawadiwa Sh. Milioni 2.

Abuu Hashim ametajwa kuwa mchezaji bora wa Mashindano  na kuzawadiwa Sh. Milioni 2.5.

Simba kwa kuwa mabingwa wa michuano hiyo mipya ya BancABC imezawadiwa hundi ya mfano yenye thamani ya shilingi milioni 40 nao Mtibwa Sugar kwa kuibuka washindi wa pili wamezawadiwa Hundi ya mfano yenye thamani ya shilingi milioni 20.

Saturday, August 18, 2012

                                 SWALA YA IDDI KITAIFA KUFANYIKA MKOANI RUVUMA WASILAMU TUJIANDAE





Swala ya Eid El Fitr na Baraza la Eid kitaifa mwaka huu vitafanyika Masjid L-huda Msikiti wa Bakwata Songea katika Mkoa wa Ruvuma.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Baraza Kuu la Waislam Tanzania Suleiman Lolila, Swala hiyo itafanyika kati ya tarehe 19 au 20 Agosti, 2012 kutegemea mwandamo wa mwezi.
Taarifa hiyo imefafanua kuwa Baraza la Eid litafanyika kati ya tarehe hizo hizo kuanzaia saa kumi kamili alasiri.
Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Mhe. Said Mwambungu.
Powered by Blogger.