Blogger Widgets December 2012 | Mfaume Kikwato JR

PALACE HOTEL

PALACE HOTEL

Vumbua Hazina chini ya kizibo

Vumbua Hazina chini ya kizibo
+255788788218

BAYPORT

BAYPORT
KOPA BAYPORT

Saturday, December 29, 2012

JOSEPH CHAMELEONE ANUSURIKA KIFO SIKU YA BOXING DAY 2012


Msanii maarufu wa nchini Uganda Joseph Chameleone na mkewe Daniela, jana walinusurika kufa baada ya mtu mmoja kuvamia nyumba hiyo akiwa na Petroli kwa lengo la kumuua msanii huyo, lakini akiwa kwenye hazma ya kutekeleza tukio hilo moto wa Petroli aliotaka kuwachoma na ndani ya nyumba ya msanii huyo uli muunguza vibaya mtu aliyetaka kufanya tukio hilo

ALIYE JARIBU KUMUUA MSAANI WA UGANDA JOSEPH CHAMELEONE AFARIKI DUNIA

Mtu huyo aliye fariki masaa mawili yaliyo pita, Akipatiwa matibabu amefaamika kwa jina la Robert Kalamagi mwenye umri wa miaka 27, mkazi wa Seguku Kampala Uganda, amefikwa na umauti baada ya kujeruhiwa vibaya na moto wa petroli ambao alikuwa akijaribu kumwagia mke wa msanii huyo,

Daniela ambaye ni mke wa Chameleone, aliwaambia wa andishi wa Habari kuwa, Asubuhi ya Boxing Day alisikia vishindo sebuleni, wakati akiwa chumbani na alipojaribu kujua ninani, aligundua ni nani alimkuta marehemu na akajaribu kumuuliza anataka nini lakini akumjibu chochote, Alisema Daniela.


Aidha mke wa Msanii huyo alimuita Chameleone, ndipo mtu huyo alichukua geleni la lita tano kwa lengo la kumwagia Daniela, kinyume na matarajio yake petroli ilimwagikia yeye na alipo washa moto, aliungua kiasi cha kufanya mtu huyo kujeruhiwa vibaya na moto huo, Daniela anasema mtu huyo aliomba msaada alipokuwa anaungua na moto huo.


Kilicho washangaza watu wengi wa nchini Uganda ni baada ya mtuhumiwa kuwaeleza Polisi alipofanyiwa Mahojiano akiwa Hospitali kuwa, yeye ni shabiki mkubwa wa msanii huyo, na kilichotokea kwake alitumwa na mtu ilikumuua msanii huyo


Hatahivyo Polisi wa nchini humo wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo kubaini kama hilo nitukio la ujambazi au alitumwa na mtu kutekeleza tukio hilo

IAMOND AUKANA U FREEMASON, AWASHANGAA WANAOENEZA KUWA KABADILI DINI


Msanii anaye Ng'ara katika Tasnia ya Muziki wa Bongo Fleva hivi sasa, Diamond Plantum amekana kushiriki wala kujihusisha na imani inayousishwa na nguvu za giza ya "Freemason", na kusikitishwa sana na watu wanao sambaza maneno ya kuwa yeye amebadili dini.

"Mimi sijawahi kujiusisha na imani ya Freemason na wala sijui juu ya hilo kabisaa, Nimelelewa katika imani ya Kiislamu na ninacho juwa nikuwa Mungu ni mmoja....Siwezi Kuwa Freemason Hata siku moja"Alisema Diamond.


Akiongea na Campasvision Diamond, alisema Zaidi ameumizwa sana na kusikitishwa sana na habari zinazo zagaa kuwa yeye kabadili dini, kitu ambacho sio kweli..alisisitiza kuwa awezi kuiacha dini yake na kuwa na imani tofauti na aliyo lelelwa na kudai kuumizwa na watu wanao eneza habari hizo, Alisema Diamond


Vijana wanaoiga na Kukopi kazi zangu, kimsingi nafrahishwa sana tena inanipa nguvu yakuwa kazi zangu zinakubaliwa  hata nawasanii wenzangu, Swala ambali linanifanya niongeze juhudi zaidi katika kuboresha kazi yangu. Alisema Diamond


Akiongelea juu ya Video Mpya ya Kesho Diamond alisema, amefurahishwa sana na Wimbo huo kwani ni miongoni mwa nyimbo ambazo Mashahiri yake hayakumpa shida kutunga kabisa kwa ilikuwa kama masihara lakini kilichotoka nikitu ambacho kimesimama. Alimalizia Diamond

Tuesday, December 18, 2012

YANGA WATAMKUMBUKA YAW BERKO


SASA rasmi, Yaw Berko amebaki historia ndani ya klabu ya Yanga. Hiyo inafuatia klabu ya St Eloi Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kuridhika naye baada ya majadribio.
Katibu wa Yanga, Lawrence Mwalusako ameiambia KIKWATOJR.BLOSPOT.COM jana kwamba kipa huyo Mghana amefuzu majaribio Lupopo na amesajiliwa moja kwa moja.
Kuondoka kwa Berko, kunatoa nafasi kwa kiungo kutoka DRC, Kabange Twite kusajiliwa katika klabu hiyo ya Jangwani, akiungana na kaka yake, beki Mbuyu Twite. Wachezaji wengine wa kigeni wa Yanga ni kiungo Haruna Niyonzima kutoka Rwanda na washambuliaji Didier Kavumbangu kutoka Burundi na Hamisi Kiiza kutoka Uganda.
Berko alijiunga na Yanga SC mwaka 2009, akitokea Liberty Proffessional ya kwao Ghana, timu ambayo ilimuibua pia Michael Essein na nyota wengine kibao wa Ghana. Aliletwa nchini na kocha wa zamani wa Yanga, Mserbia Kostadin Bozidar Papic aliyewahi kupiga kazi Ghana katika klabu ya Hearts POf Oak.
Alikuwa kipa bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Bara msimu wa 2010/2011 na katika kipindi chake cha kufanya kazi Jangwani, anajivunia kuiwezesha timu kutwaa mataji ya ubingwa wa Bara msimu wa 2010/2011 na Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame mara mbili mfululizo, 2011 na 2012.
2011 alidaka mechi zote, lakini 2012 alidaka hadi Robo Fainali alipoumia na kumuachia Ally Mustafa ‘Barthez’ aliyedaka hadi ubingwa. Yanga imeridhika na uwezo wa Barthez langoni iliyemsajili kutoka Simba msimu huu na kuamua kuachana na Berko, ambaye alikuwa kipenzi cha wapenzi wa klabu hiyo.
Awali, Yanga ilijifikiria mara mbili kuachana na Berko, kwa kuhofia Barthez angeanza ‘kuwaringia’ kwa kuona amebaki peke yake kipa bora, lakini imepanga kumhamasisha Said Mohamed kuimarisha kiwango chake, vinginevyo atatemwa mwishoni mwa msimu.
Na Yanga imekuwa na ‘jeuri’ ya kumtema Berko baada ya kuona mwakani haitashiriki michuano ya Afrika, zaidi ya Ligi Kuu na jukumu la kwenda kutetea taji lake la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame mjini Kigali, Rwanda.
Japokuwa anaondoka, lakini kwa uhodari wake langoni, Berko atabakia kwenye kumbukumbu ya mashabiki wa Yanga.

WASIFU WAKE:
JINA: Yaw Berko
KUZALIWA: Oktoba 13, 1980
ALIPOZALIWA: Accra, Ghana
KLABU ZA AWALI:
Mwaka               Klabu
2000-2005:        Liberty Professional   
2005-2006:        Pisico Binh Dnh F.C. (Vietnam, mkopo)  
2006-2009:        Liberty Professional   
2009- 2012:       Yanga SC
2012:                 St Eloi Lupopo 

Thursday, December 13, 2012

sharoo pengo lakoo bado haliwezi zibika mungu akubariki


Ni watu wengi wamehitaji kufahamu kuhusu kauli ya familia ya Marehemu mwigizaji/msanii Sharo Milionea baada ya tangazo la Airtel lenye sauti yake kuendelea kutumiwa na kampuni hiyo wiki kadhaa baada ya Sharo kufariki kwa ajali ya gari iliyotokea novemba 26 2012 Tanga.

Mjomba wa Marehemu ambae ndio msemaji wa familia Shaban Mkiete amethibitisha kwamba wamezungumza na kukubaliana na kampuni ya Airtel na hapa namkariri akisema “ni kweli tumekubaliana, kwa mujibu wa mkataba wao lilikua linaisha terehe 31 mwezi huu tumekubaliana kwamba liendelee kwa makubaliano ambayo tumekubaliana nayo sisi kati ya mzee Majuto ambae bado yupo na familia ya Marehemu, mama mzazi wa Sharo Milionea ameridhia hilo hakuna tatizo”

Siku ya msiba kikwatojr.blogspot.com ilipopata nafasi ya kuongea na mwakilishi wa Airtel alisema Marehemu Sharo Milionea alifariki ndani ya kipindi cha miezi 6 tu toka asaini dili la kuwa balozi wa Airtel na kufanya matangazo mbalimbali yeye na mzee Majuto.
                                     
Sio tu dili la Airtel, imefahamika tayari Sharo Milionea alikua amesaini mikataba mizuri na makampuni mbalimbali wakiwemo Wamarekani waliotengeneza filamu maarufu Afrika kama Yellow Card, Neria na nyingine ambapo kwa sasa Wamarekani hao wako hapa Tanzania na wametengeneza series kadhaa ikiwemo Wahapahapa na Siri ya Mtungi ambayo ndio Sharo Milionea kashiriki ndani na mpaka anafariki tayari alikua ameshaanza kucheza igizo hilo.

Monday, December 10, 2012

katika kuelekea sikukuu za x-mass na mwaka mpya viongozi mbalimbali wawatakia wananchi wao heri za sikukuu hizo

Mkuu wa wilaya ya mkinga mkoani Tanga Bi Mboni Mgaza wakati akiweka jingo katika Production za redio Mwambao Fm Tanga za kuwatakia mafanikio mema ya X mass na Mwaka Mpya wananchi wa wilaya yake ya mkinga

Hapa akiwa anapewa maelekezo na baadhi ya watangazaji wa redio mwambao fm jinsi ya kutia sauti za kuwatakia heri wananchi wa wilaya ya mkinga na mkoa wa tanga kwa ujumla.



picha ni Badhi ya watangazaji wa redio mwambao fm kuanzia kushoto ni Kalonga Kasati katikati ni mkuu wa wilaya ya Mkinga Bi Mboni Mgaza  wapili kutoka kwa mkuu wa wilaya ni Selemani Kibugo huku wamwisho ni kijana Almasi Shija  wakiwa katika picha ya pamoja mara bada ya kukamilisha mandalizi ya jingo za X Mass na Mwaka Mpya Kwa upande wa viongozi wa mkoa watanga kwa ujumla.

Mkurugenzi wa Blog ya kijamii ya Kikwatojr.blogspot.com anawatakia wale wote wanao tembelea blog hii ya kijamii kwa lengo la kupata habari mbali mbali na kimaendeleo Heri ya X Mass na Mwaka Mpya wadau wanguu wote nawapenda sana na nimewandalia mambo mazuri kwa mawaka wa 2013 cha msingi usisite kutembelea blog hii ya kijamii 

Saturday, December 1, 2012

Mali za Sharo Milionea zasalimishwa

Baadhi ya vitu vya marehemu Sharo milionea vilivyokamatwa baada ya msako mkali baina ya Polisi na wananchi wa Kijiji Songa Kibaoni vikiwa katika kituo cha polisi chumbageni  jijini Tanga.

vitu hivyo  vilivyoporwa na watu wasiojuliana katika ajali ya msanii mahiri wa 

filamu na muziki wa kizazi kipya nchini, Marehemu Hussein Mkieti ‘Sharo 

Milionea’ eneo la Songa Kibaoni wilayani Muheza mkoani Tanga, vimesalimishwa na wananchi wanaosadikiwa ni wezi.

Kwani alikuwa akitokea Jijini Dar es Salaam kuelekea kijijini kwao Lusanga 

Muheza, kwa dhumuni la kwenda kuwasalimia wazazi wake pamoja na kuwapelekea fedha za matumizi.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe, jana

 alithibitisha kupatikana vitu hivyo, ambako alisema upatikanaji wake ulitokana 

na msako mkali uliofanywa na uongozi wa serikali Muheza wakishirikiana na
Jeshi la Polisi wilayani humo.

Alisema kwamba baada ya kutokea kwa tukio hilo, Jeshi la Polisi mkoani Tanga, liliweka mtego na kutangaza kuinunua simu ya mkononi ya msanii huyo aina ya 

‘blackberry’ ndipo moja kati ya wanaodaiwa vibaka waliohusika kwenye tukio hilo, alipojitokeza na kuipeleka kwa ajili ya kuiuza.

Kwani walipofika eneo ambalo walikubaliana, walikabidhi simu hiyo kwa ajili ya kuikagua, lakini baadaye wezi hao walishtukia mtego huo na kukimbia huku
 wakiiacha simu hiyo.

Aidha, Kamanda Massawe alivitaja vitu ambavyo vimesalimishwa kwa jeshi hilo 

kuwa ni simu ya mkononi aina ya blackberry, Betri la gari, tairi la akiba, radio 

ya gari, begi ambalo lilikuwa na nguo za marehemu, saa ya mkononi na nguo 

ambazo alikuwa amevuliwa na vibaka wa eneo hilo mara baada ya kutokea ajali hiyo.

Mpaka kufikia sasa, msako unaendelea na wamebaini baadhi ya washukiwa wa 

uhalifu huo wamezikimbia nyumba zao kwa hofu ya kukamatwa.

Polisi wako kwenye uchunguzi mkali ili kuhakikisha wanawatia mbaroni wale 

wote ambao waliohusika na kitendo cha kinyama, alichofanyiwa msanii huyo.



Powered by Blogger.