Blogger Widgets September 2012 | Mfaume Kikwato JR

PALACE HOTEL

PALACE HOTEL

Vumbua Hazina chini ya kizibo

Vumbua Hazina chini ya kizibo
+255788788218

BAYPORT

BAYPORT
KOPA BAYPORT

Sunday, September 30, 2012

wavamizi wa maeneo wilayani kilindi na handeni kutakiwa kuondoka haraka

MKUU wa mkoa wa Tanga lutein mstaafu Chiku Gallawa amewataka watu waliohamia wilayani Kilindi na Handeni mkoani Tanga kuondoka katika wilaya hizo, ili kupisha walengwa ambao ni wazawa wa wilaya hizo, nakwamba amefikia uwamuzi huo kutokana na wahamiaji hao kuhodhi aridhi kinyume na taratibu za kisharia.
Uamuzi huo ameutoa katika kikao cha kamati ya ushauri mkoa wa Tanga RCC kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano katika ofisi ya mkuu wa mkoa
Aidha mkuu huyo wa mkoa lutein Gallawa amesema kwamba Kilindi na Handeni sio shamba la wavamizi hivyo ni vema wakazi hao ambao wamehamia kinyume na utaratibu wa kisharia kuondoka katika maeneo hayo haraka iwezekanavyo kabla ya kufika mwezi Januari mwakani  ili kuepusha vurugu na migogoro ya aridhi siokuwa na tija mkoani hapa.
Hata hivyo mkuu huyo wa mkoa wa Tanga amewataka wakurungenzi wa halmashauri zote mkoani hapa kusimamia majukumu yao ipasavyo ili kukomesha hali hiyo kwa kuwatambuwa wazawa halali katika halmashauri zao.
Na katika hatua nhyingine amewataka wakurungenzi hao watumie wanasheria wao katika Halmashauri zao ili kutambua sharia za uchimbaji wa Madini kuliko kuchimba madini kiholela bila kuwa na utaalamu jambo ambalo mara nyingi limekuwa likileta athari kubwa kwa wananchi bila kupata faida yeyote katika maeneo husika.
Kufuatia hali hiyo lutein Gallawa wamewashauri wakurungenzi na wakuu wa wilaya kuwa na idadi maalumu ya wachimba madini ili kuondoa fujo kwa wananchi ikiwemo kuwapa vibali maalum pamoja na risiti.

pangani sasa kupata matunda ya mbunge wao


MBUNGE wa Pangani Bw Salehe Pamba ametoa msaada wa bati 80 kwa Shule ya msingi Kilimangwido kutokana na shule hiyo kuchakaa paa lake na kuleta adha kubwa kwa wanafunzi wa shule hiyo.
Hatua hiyo ya Mbunge inakuja kufuatia ziara zake za hivi karibuni kubaini uchakavu wa shule hiyo ambapo awali wanafunzi walikuwa wakinyeshewa na mvua nyakati za masika na kudumaza kiwango cha elimu.
Alisema juhudi hizo ni utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuwasihi wananchi wa Pangani kuendelea kukiunga mkono chama hicho kwani kinatekeleza ahadi zake kwa vitendo kwa lengo la kuwaletea wananchi maendeleo.
Akikabidhi msaada huo jana kwa Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bw Albert Bukulu  Mbunge huyo aliwataka wananchi wa jimbo hilo kuendelea na mshikamano walionao katika kuchangia shughuli  ikiwemo elimu ili kupiga hatua kubwa  za maendeleo ya jimbo hilo.
Bw Pamba alisema wakati umefika wa wananchi kuthamini elimu kwani ndio chimbuko la maendeleo ya jamii hiyo na kuwasisitiza wazazi umuhimu wa kupeleka shule watoto wao.
Akipokea msaada huo Bw Bukulu alisema umekuja wakati muafaka ambapo wanafunzi walikuwa wakipata tabu kutokana na uchakavu wa majengo hayo na kushukuru juhudi za MBunge huyo kuthamini elimu.
Alisema kitendo cha Mbunge huyo kutoa msaada huo ni wazi anatambua kuwa elimu ndio msingi wa maendeleo ya jamii na kumhakikishia kuwa msaada huo utasaidia kuchochea kasi ya elimu katika shule hiyo.
Mbunge huyo anaendelea na ziara yake ya kusikiliza kero za wananchi na kuendelea kuunga mkono juhudi mbalimbali za maendeleo yanayofanywa na wananchi wa jimbo hilo.


TANZANIA imetenga kiasi cha shilingi bilioni 30 kwa ajili ya
kuendeleza kilimo hasa kuwainua wakulima wa vijijini ambao
wanakabiliwa na changamoto kubwa ya wataalamu na maafisa ugani  wa
Hayo yalisemwa jana na waziri wa kilimo chakula na ushirika Tanzania
Christopher Chiza alipokuwa akifunga mkutano wa wadau wa sekta ya
kilimo  wa mapinduzi ya kijani uliomalizika jana  mjini hapa.
Alisema kuwa Tanzania bado inakabiliwa na changamoto kubwa ya
kukosekana kwa  wataalamu wa kilimo hali inayopelekea wakulima
wadogowadogo hasa wa vijjiini kulima kilimo cha mazoea ambacho hakina
tija kwao .
Aidha alifafanua kuwa kutokana na changamoto hiyo ya kukosekana kwa
wataalamu wa kilimo wakiwemo  maafisa ugani imekuwa ni sababbu kubwa
ya Tanzania kutofikia katika malengo yake muhimu waliyojiwekea hasa
katika sekta ya kilimo .

“Tanzania bado tunakabiliwa na changamoto ya wataalamu wa kilimo na
hii inasababisha wakulima kuendelea tu na  kilimo ambacho hakina tija
yeyote kwao  hivyo hii bajeti tuliyoitenga tutahakikisha wakulima
wanafikiwa na elimu ambayo itawafanya wapige hatua katika kilimo na
pia kupukana na kilimo cha mazoea”alisema Chiza
Kutokana na hali hiyo waziri chiza alisema kuwa kutokana na bajeti
ambayo Tanzania imetenga watahakikisha kuwa maafisa ugani na wataalamu
watapatikana wa kutosha ili iweze kutolewa  elimu ya kutosha kwa
wakulima ambao wanalima kilimo cha mazoea ili waweze kuondokana na
hali hiyo.
Kwa upandea wake waziri wa maji profesa Jummane  Magembe alisema kuwa
kwa sasa kuna uharibifu wa vyanzo vya majiunaotokana na kuchoma misitu
kwa ajili a kilimo ,mila potofu ,uwindaji,kufyeaka maeneo ya vyanzo
,kuchoma mkaa  hivyo kusababisha kutokea kwa mabadiliko ya tabia nchi
ambayo yamekuwa yakiathiri kilimo  cha Tanzania.
Magembe aliongeza kuwa ni vema watanzania wakajikita zaidia katika
kutumia nishati ambazo hazichangii kuleta uharibifu wa mazingira kama
vile nishati ya umeme wa jua ambapo endapo wananchi watatumia nishati
hizo ni wazi kuwa mabadiliko ya tabia ya nchi hayatakuwepo tena

Friday, September 28, 2012

hivi ndivyoo vijana wetu wanavyo dangavywa?

LINAH ajitoa rasmi THT!

Baada ya kupata mafanikio makubwa toka nyumba ya vipaji Tanzania msanii Lina Sanga, ‘Linah’ amesema kwa sasa atakuwa nje ya Taasisi hiyo baada ya kufanikisha kumuweka juu kimuziki.
Akizungumza na Darhotwire jana Linah alisema atafanya kazi zake peke yake, ingawa atakuwa mwepesi kupata ushauri kutoka kwa walioibua na kuendeleza kipaji chake.
Alisema kujiweka kando kwa taasisi hiyo, ni sababu ya kuwapa nafasi wasanii wengine wachanga waliokuwa ndani ya THT ili waendelezwe na kuwa kama yeye.
Alisema ni kweli THT imemlea vizuri hadi kufikia alipokuwa sasa, hivyo kwa kuwa ameshafika hatua nzuri, ni sababu ya kuleta chachu kwa wasanii wengine waliokuwa na malengo ya kuwika katika nyanja za Kimataifa.
“Nimekuwa nje ya THT kama mwanzo mzuri wa kujitegemea katika ulimwengu wa muziki hapa nchini, ingawa naamini bado nitakuwa mwepesi kuomba ushauri na mabosi wangu hao au kupata kazi kutoka mahali popote.
“Nimeondoka kama sehemu ya utaratibu wa THT kuwapa uhuru wasanii waliofanikisha ndoto zao ili kutoa nafasi kwa wasanii wengine, ukizingatia taasisi hiyo imesheheni waimbaji wachanga wengi na wenye ndoto za kufikia malengo,” alisema.
Wasanii wengine waliofikia malengo yao wakiwa ndani ya taasisi hiyo ni pamoja na Barnabas, Mataruma, Amini, Mwasiti, Linex na  Ditto.

Swahili Kwenye simu Matangazo Sudan mbili zasaini makubaliano










Sudan na Sudan Kusini zimetia saini makubaliano kuhusu biashara, mafuta na usalama ingawa hazijakubaliana kuhusu mipaka.
Baada ya mazungumzo ya siku ya nne, nchi hizo mbili zimeafikiana kuruhusu usafirishaji wa mafuta kutoka kusini kupitia mabomba ya Kaskazini na kuondoa wanajeshi mpakani.
Viongozi wa nchi hizo mbili hatimaye wamekubaliana baada ya mazungumzo ya siku nne mjini Addis Ababa Ethiopia.
Lakin maswala kadhaa muhimu yangali kutatuliwa ikiwemo kuafikia makubaliano kuhusu mipaka inayozozaniwa ikiwa ni mojawpao ya kilichosababisha mgogoro ambao nusura utumbukize nchi hizo kwenye vita mapema mwaka huu.
Baada ya mapigano kuzuka kuhusu mzozo wa mafuta na mipaka, Umoja wa mataifa ulitishia kuziwekea pande zote mbili vikwazo ikiwa hazitaafikia makubaliano ya kina.
Wapatanishi wa Muungano wa Afrika wangali kuthibitisha kuwa makubaliano yameafikiwa lakini rais wa Sudan Omar al-Bashir na mwenzake wa Kusini Salva Kiir, wanatarajiwa kutia saini makubaliano hayo hii leo.
Maelezo yametolewa tu kwa mukhtasari lakini wapatanishi wa pande zote mbili, walisema kuwa wamekubaliana kuhusu eneo la nchi hizo mbili ambalo halina ulinzi wa kijeshi.
Pia makubaliano ya kiuchumi yaliafikiwa kuruhusu Sudan Kusini kuanza tena shughuli zake za kuzalisha mafuta.
Lakini mwafaka haukupatikana kuhusu eneo linalozozaniwa la Abyei wala mipaka mingine mingi ambayo nchi hizo zinazozania.
Kwa hivyo makubalino hayo hayajaweza kutimiza masharti ya Umoja wa Mataifa kwa nchi hizo kuafikia mkataba unaotatua mzozo huo kwa kina.

Majeshi ya AMISOM yaingia Kismayo

 

Hatimaye wanajeshi wa Kenya wameuteka mji wa Kismayo.
Wanajeshi wa Kenya walifanikiwa kuingia mji huo baada ya kukabiliana vikali na wapiganaji wa kundi la Al Shabaab.
Msemaji wa jeshi la Kenya Kanali Cyrus Oguna aliambia blog hii  kuwa wanajeshi wa Kenya kwa ushirikiano na wale wa Somalia walianza harakati zao mapema asubuhi ya leo.
Aliongeza kuwa hadi kufikia sasa Al Shabaab hawajakabiliana na jeshi hilo kuzuia kutekwa kwa mji huo.
Lakini mwandishi wa BBC anasema kuwa Al Shabaab husalimu amri kwa muda wakati wanapokabiliwa na majeshi yenye nguvu kuwaliko.
Ndege za kivita za Kenya zilifanya mashambulizi ya angani mapema wiki hii na kuharibu boharli lenye silaha za wapiganaji hao mjini humo.
Wiki iliyopita, Al Shabaab walijiandaa kuondoka Kismayo na hata kuwahamisha wapiganaji wao pamoja na silaha.
Mji huo wa bandarini ni muhimu kwa Al Shabaab kwani wanautumia kuingizia silaha na pia kuwatoza kodi wenyeji wa mji huo.
Hatua ya wao kupoteza mji huo, itakuwa ni pigo kubwa kwao, lakini wapiganaji hao wa Al Shabaab bado wana uwezo wa kufanya mashambulizi dhidi ya wanajeshi wa Somalia na wale wa Muungano wa Afrika hata katika sahamu ambazo wanajeshi hao wanadhibiti.

WANAWAKE WA BONGO MOVIE WANAPENDA KUMEGWA NA WANAUME WANAOUZA MADAWA YA KULEVYA WAKIDHANI WATATAJIRIKA ” – SHILOLE…!! 

WAKATI wasanii wengi wakishindana kwa kubadilisha magari ya kifahari hapa mjini, msanii wa filamu na muziki Shilole, amefunguka na kudai kuwa kuna kasoro kubwa hasa ya kiumaskini kwani wanawake wengi wa bongo movie wanapenda kumegwa na wanaume wanaofanya biashara haramu ya madawa ya kulevya kwa kudhani kuwa watapewa dili la kulala maskini na kuamka tajiri.

Wapo wasanii wengi ambao wanajisifu kwa kuwa na magari ya kifahari lakini ukitazama kwa hali ya kawaida gari analiotembelea na thamani ya hela anayolipwa katika kila filamu wala haviendani.


Shilole
alidai kuwa kasoro hiyo inasababishwa na tamaa za baadhi ya wasanii kwani wanaamini wakitembea na wanaume wanaofanya biashara hizo nao wanaweza kufanikiwa mapema huku wakisahau kuwa riziki hutoa Mungu na si binadamu yeyote yule.

Msanii huyo alidai kuwa wapo baadhi ya wasanii ambao wamefanikiwa si kwa kuwatengemea wanaume, lakini asilimia kubwa wanakaa na kujipendezesha wakisubiri mwanaume ndiye wawafanyie kila kitu eti kwa sababu ya umaarufu wao.


“Hata siku moja uji kusikia eti Shilole anaishi mjini kwa sababu mtu ya fulani .Mi ni jembe nimekuja mjini kutafuta na si kutafutiwa kama wasanii wengine wanasubiri kupata mwanaume anayefanya biashara harumu ili nao wamepewe dili la kulala maskini na kuamka na tajiri,”
alidai.

Hata hivyo aliongeza kuwa wanawake wengi wanatumia miili yao kama sehemu moja wapo ya kujiigizia kipato huku wakisahau kuwa kuna magonjwa hatari kama Ukimwi na mengine mengi.

COASTAL UNION WAGOSI WAKAYA SASA NAFASI YA PILI KATIKA MSIMAMO WA LIGI KUU YA VODACOM BARA! 

Coastal Union 2012 Tunatisha......Ndio Inavyosomeka.Mmoja wa Shabiki wa Coastal Union Akitoa ujumbe wake Kwa njia ya Bango.
Mechi 4 points 8=Nafasi ya 2
Ni Balaaaaaaaaaaaaaa!!!
Na sasa tunakamata nafasi ya pili.........,Hii ndio raha ya ushindi......!!! Photo: Coastal Union 2012 Tunatisha......Ndio Inavyosomeka.Mmoja wa Shabiki wa Coastal Union Akitoa ujumbe wake Kwa njia ya Bango.
Mechi 4 points 8=Nafasi ya 2
Ni Balaaaaaaaaaaaaaa(LIKE)

Monday, September 24, 2012

kibonzo cha leo wadau tafakari chukua hatua?



kwa halii hiii kwelii tutaweza kuzibiti uhalifuu

SIMBA YAIONESHA RUVU SHOOTING 2-1 WANJA WA TAIFA

 


(Kipa wa timu ya Ruvu Shooting Benjamin Haule akipangua mkwaju wa penalti uliopigwa na Mshambuliaji wa Simba Daniel Akuffor wakati wa mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Picha na Jackson Odoyo.)

MSHAMBULIAJI wa Simba Daniel Akuffor, amekosa penalti wakati wa mechi  ya Ligi Kuu tanzania Bara,  inayoendelea hivi sasa katika Uwanja wa Taifa jijini
Dar es Salaam, Mshambuliaji huyo alikosa penalti hiyo katika dakika 45 kipindi cha kwanza.
Mwamuzi wa mchezo huo Roanald Swai, aliamuru ipigwe penalt hiyo baada ya beki wa Ruvu Shooting kunawa mpira ndani ya 18.
Awali kabla ya mshambuliaji huyo  raia wa Ghana kukosa penalti hiyo, Simba  ilikua inaogoza kwa bao 1-0 iliyofungwa na  Felix Sunzu kwa kichwa.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kila timu ikihitaji ushindi, ambapo Ruvu Shooting ndiyo iliyokuwa ya kwanza kupata goli la kusawazisha, lillilofungwa na Self Rashid dakika 75 akitokea benchi baada ya kuunasa mpira uliopigwa na beki wa Simba Nassoro Masoud (Cholo), dakika ya 80 ya mchezo mshambuliaji Kinda wa Simba aliyeingia kuchukuwa na nafasi ya Daniel Akuffor Edward Christopher alifunga bao la pili baada ya kupata pasi safi ya Mrisho Ngassa.mpaka dakika 90 Simba 2-Ruvu Shooting 1.

Baby Madaha atua na 'Nimezima'

Mwanamuziki huyo alisema kwamba kwa sasa yupo kwenye hatua za mwisho 'za majeruhi', kuisuka albamu hiyo itakayobeba nyimbo nane.
Si mwingine bali ni yule Msanii wa Muziki wa kizazi kipya, Baby Joseph Madaha ‘Baby Madaha’, anajipanga kuachia albamu yake ya pili inayokwenda kwa jina la ‘Nimezama’.
Kwani mipini iliyomo kwenye albamu hiyo mpya, iko tayari na ameanza kuzifanyia video ili kuwapa raha mashabiki wake.
Ndani ya albamu hiyo nyimbo ambazo amemaliza kuzifanyia video ni chache, kwani bado anaendelea na kazi ambayo naamini mashabiki wake wataipenda kulingana na ujumbe na ubora wake.
Mbali na hilo mwanamuzki huyo amewataka mashabiki wake, waendelee kumpa sapoti kwenye kazi zake kwani kuna vitu vingi ambavyo amewaandalia, wasicheze mbali na yeye.

Friday, September 21, 2012

Maandamano dhidi ya filamu chafu ya kumkashifu mtume yaendelea duniani kote

Maandamano ya kupinga filamu ya Kimarekani na vijikatuni vya Kifaransa vinavyomvunjia heshima Mtume Muhammad (saw) yameendelea kufanyika katika nchi mbalimbali duniani.
Mjini Tehran maelfu ya watu waliandamana jana mbele ya ubalozi wa Ufaransa wakipiga nara za "mauti kwa Marekani", "mauti kwa Israel"  "mauti kwa Ufaransa" na "mauati kwa Uingereza".
Maandamano makubwa kama hayo yamefanyika pia nchini Afghanistan kupinga vijikatuni hivyo na filamu ya Kimarekani inayomtusi Mtume wa Mwenyezi Mungu. Waandamanaji hao wametaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya watengenezaji na watayarisha wa filamu na katuni hizo.
Huko Pakistan maelfu ya Waislamu wameandamana katika miji ya Islamabad na Lahore wakilaani hujuma za Wamagharibi dhidi ya Uislamu. Polisi wa Pakistan walizuia waandamanaji hao kuvamia ubalozi wa Ufaransa na inaripotiwa kuwa karibu waandamanaji hamsini wamejeruhiwa.
Maandamano makubwa ya kulaani filamu ya Kimarekani na vijikatuni vinavyomvunjia heshima Mtume wa Mwenyezi Mungu yanatazamiwa kufanyika leo katika maeneo mbalimbali ya dunia kabla na baada ya swala za Ijumaa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amejaribu kutuliza hasira za Waislamu akisema kuwa filamu ya Kimarekani ya "Innocence of Muslims" inaaibisha na kukera. Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kuwekwa mipaka ya uhuru wa kujieleza na kusema unaotumiwa vibaya kushambulia itikadi na matukufu ya Kiislamu.

JK amua sasa kuzinduzi ujenzi daraja la Kigamboni

NewsImages/6606294.jpg 
(picha raisi kikwete akizindua jiwe la msingi)
 Rais Jakaya Kikwete, alizindua rasmi ujenzi wa daraja hilo jijini Dar es Salaam

Daraja hilo litakuwa na urefu wa mita 680 na litakuwa na jumla ya barabara sita ambazo, ambapo daraja hilo litaunganisha maeneo ya Kigamboni na Kurasini

Rais Jakaya Kiwete aliwaomba wakazi wa kigamboni ambao mradi umewafuata wasiwe na wasiwasi wkani stahiki zao zipo na tayari zimeshatayarishwa

Na kuwatahadharisha wakazi wengine ambao wana mpango wa kujenga wasimamishe ujenzi kwani hao hawataweza kulipwa kwa kuwa zuio la ujenzi lilishatolewa

Amesema lengo la Serikali ni kuifanya Kigamboni kuwa mji mpya na wa aina yake ikiwemo na kuboresha jiji la Dar es Salaam.

Pia Rais Kikwete alikana uzushi na uwongo uliozushwa kwamba amemuuzia mji wa Kigamboni Rais wa zamani wa Marekani George Bush kuwa ni uzushi

“Iweje nimuuzie Bush kwanza afate nini huku, yeye ni watu matajiri, kuna watu wanataka wachafue nchi kwa k maslahi yao”

Naye Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli amesema pindi daraja hilo litakapokamilika, watembea kwa miguu na baiskeli ndiyo ambao hawatatozwa kutumia daraja hilo, bali wengine wote watatozwa kwa ajili gharama za uendeshaji wa daraja.
Amesema ujenzi wa daraja hilo linatarajiwa kukamilika mwishoni m

kaliya mwaka wadauuu kwa vijana wetu walio maliza darasa la saba

Msichana huyo [14] jina limehifadhiwa, ambaye alikuwa akifanya mtihani wake wa darasa la saba, alianzwa na hali ya uchungu akiwa katika chumba cha mtihani na hatimaye kujifungua mtoto

Awali ilidaiwa kuwa, mwanafunzi huyo alimuomba msimamizi wake aende msalani akajisaidie na msimamizi huyo alimruhusu, hivyo kudaiwa baada ya dakika chache alimuomba tena msimamizi huyo ruhusu aende nje lakini ilidaiwa msimamizi hakumruhusu kwa kudhani huenda mwanafunzi huyo alikuwa anafanya ujanja wa kupata majibu ya mitihani

Imedaiwa msimamizi huyo alimzuia mwanafunzi huyo asitoke lakini baadae msimamizi huyo alianza kuingiwa na wasiwasi kwa kuona binti huyo anajinyonga zaidi na kumuuliza anasumbuliwa na nini na mwanafunzi kudaiwa alimjibu anasumbuliwa na tumbo

Lakini jibu hilo halikumtosheleza msimamizi huyo kwa kuona msichana huyo anazidi kujinyonga nyonga, aliendelea kumuuliza linamuuma vipi ndipo mwanafunzi huyo alimwambia ukweli msimamizi huyo kwa kumwambia anaumwa na uchungu

Msimamizi huyo ndipo alipoanza kufanya juhudi za kutafuta msaidizi ili wamsaidie binti huyo lakini baadae binti huyo alifanikiwa kujifungua mtoto wa kiume akiwa katika chumba hicho

Taarifa hizi zimethibitishwa na uongozi wa shule ikiwemo Afisa Elimu wilayani humo akiwemo Mkurugenzi Halmashauri ya Kagera

Tuesday, September 18, 2012

Mke wa Mjukuu wa Mandela Apewa Mimba na Kaka Yake

Mjukuu wa rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela amelazimika kumuacha mkewe baada ya mke wake huyo kupata mimba na baadae kujifungua mtoto kufuatia uhusiano wa siri wa kimapenzi na kaka wa mjukuu huyo wa Mandela.

Mandla Mandela ambaye ni mjukuu wa aliyekuwa rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, amemfukuza mke wake mrembo wa Ufaransa, Anais Grimaud baada ya kugundulika kuwa mtoto aliyejifungua mwezi septemba mwaka jana si wa kwake.

Vipimo vya DNA vilithibitisha kuwa mtoto huyo hakuwa mtoto wa Mandla hivyo kupelekea familia ya Mandela kuamua mwanamke huyo arudishwe kwao kwa kuitia aibu familia hiyo.

Kali ya yote ni kwamba Anais anadaiwa kupewa  mimba hiyo na kaka yake Mandla kufuatia uhusiano wao wa siri wa kimapenzi wakati Mandla alipokuwa safarini.

"Familia ya Mandela imeamua kumrudisha Nkosikazi Nobubele Mandela (nee Anais Grimaud) kwa familia yake baada ta kugundulika kuwa alikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na mmoja wa kaka zangu".

"Nathibitisha kuwa uhusiano huo nje ya ndoa ulipelekea kuzaliwa kwa mtoto Qheya mwezi septemba mwaka jana" ilisema sehemu ya taarifa ya mjukuu huyo wa Mandela.

Baada ya kuzaliwa kwa mtoto huyo mwaka jana, Mandla na Mkewe walimkabidhi mzee Mandela mtoto huyo na Mzee Mandela alimpa jina mtoto huyo katika sherehe iliyofanyika septemba 16 mwaka jana.

Wakati Mandla Mandela akidai kuwa mtoto huyo ni wa mmoja wa kaka zake, Ndaba Mandela ambaye ni mshukiwa mkubwa wa kutembea na mke wa mdogo wake alikanusha kuwa mtoto huyo si wake.

"Hakuna mtu anayemjua baba wa mtoto huyu, naweza kuongea kwa kujiamini kuwa mimi sio baba wa mtoto huyu", alijitetea Ndaba Mandela.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Mandla alisema kuwa amehuzunishwa sana na kugundulika kwa mkewe kutembea nje ya ndoa.

"Kugundulika kwa mapenzi haya nje ya ndoa kumekuja kama mshtuko mkubwa sana kwangu na familia yangu. Nimehuzunishwa zaidi kwakuwa kaka yangu mwenyewe ndio mtuhumiwa mkubwa wa kunisaliti", alisema Mandla Mandela katika taarifa yake.

Aliyetengeneza Filamu ya Kumkashifu Mtume aingia machimboni

Nakoula Basseley Nakoula, ambaye ni tapeli mwenye kujipa majina mbalimbali mwenye umri wa miaka 55 ambaye alihukumiwa kwenda jela miezi 21 nchini Marekani kwa makosa mbalimbali ya utapeli mwaka 2010, ameingia mafichoni pamoja na familia yake baada ya maandamano ya kuipinga filamu aliyoitengenza kuzidi kupamba moto.

Nakoula alijiita jina la Sam Bacile wakati wa utengenezaji wa filamu ya "The Innocence of Muslims" ambayo trela lake liliwekwa kwenye YouTube na video zake zikimuonyesha mtu aliyeigiza kama mtume Muhammad, akifanya mapenzi, akibaka na akiamuru kuuliwa kwa watu.

Nakoula aka Sam Bacile hajaonekana tangu jumamosi baada ya polisi kwenda nyumbani kwake kumhoji na familia yake ya watu wanne nayo jana jumatatu iliihama nyumba yao na kwenda mafichoni kujiunga na Nakoula.

Polisi wa Los Angeles waliwasili majira ya alfajiri kabla jua halijachomoza na walimchukua mke wa Nakoula na watoto wake watatu na kuwasindikiza kwenye maficho ya siri ambako Nakoula amejificha.

Familia yake ilizificha sura zao wakati wakisindikwa na polisi toka kwenye nyumba yao iliyozungukwa na waandishi wa habari wengi waliokuwa wakikesha mbele ya nyumba hiyo.

"Waliona kuwa watakuwa salama sehemu ambayo wataweza kutoka nje na kuishi maisha ya kawaida", alisema msemaji wa polisi na kuongeza "Tulichokifanya sisi ni kuwachukua na kuwapeleka sehemu ambayo Nakoula amejificha".

Nakoula aliwahi kutupwa jela miaka miwili iliyopita kutokana na utapeli wa cheki za watu kwa kutumia majina mbalimbali feki. Alikaa jela mwaka mmoja kabla ya kutolewa kwa masharti kumalizia kifungo chake uraiani.

Vyombo vya habari vya Marekani vimekuwa vikiripoti kuwa kujihusisha kwake kutengeneza filamu hiyo kunaweza kukawa kumevunja masharti aliyopewa hivyo anaweza kurudishwa jela.

Monday, September 17, 2012

kicheki kitu cha kijana stamina akiwa na darasa ngoma imakwenda kwajina tamaa

ngoma iko powa chamsingi wadau mpeni sapati ya kutosha kija kwani anaweza na anafanya kazi powa sana

Bweni la wanafunzi lawaka moto Njombe

Zaidi ya wanafunzi 93 wa kidato cha tatu na nne katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Wanike mkoani Njombe, wamenusurika kifo baada ya bweni lao kuteketea kwa moto.
 
Mkuu wa Wilaya ya Wang’ing’ombe, Esterina Kilasi, alisema tukio hilo lilitokea Septemba 13, mwaka huu saa 4:00 usiku.

Alisema moto huo uliteketeza vifaa mbalimbali  vya wanafunzi.

Hata hivyo, alisema moto huo hakuleta madhara kwa upande wa wanafunzi na thamani ya vifaa pamoja na chanzo cha moto huo havijafahamika.
chanzo zaidi blog ya kikwatojr inaendelea kukichunguza na itakapo kipata tutawafahamisha zaidi

 

hiki nikile kichupa cha kwake wakuitwa bibi cheka akiwa na nunda mh tembeleee. ngoma inaitwa ninwewe


hiki nikile kichupa cha kwake wakuitwa bibi cheka akiwa na nunda mh tembeleee. ngoma inaitwa ninwewe


 LINEX  SASA KUAMUA KUACHIA NGOMA YA NTAIFICHA KIDEONI

 

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Sunday Mangu ‘Linex’, anajipanga kuachia video ya wimbo wake unaokwenda kwa jina la ‘Ntaificha wapi’ ambayo inafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Linex alisema ndani ya wimbo huo kamshirikisha mkali wa muziki wa bongo fleva nchini, Naseeb Abdul ‘Diamond Pletinum’.

Linex alisema anaamini wimbo huo utafanya vizuri katika  soko la muziki na uwepo wa Diamond katika wimbo huo kutamsaidia yeye kuvuta mashabiki wengi kutokana na msanii huyo kupendwa na mashabiki wengi.

“Penye ukweli inatakiwa tuseme ukweli, Diamond ni msanii ambae anakubalika katika soko la muziki si ndani wala nje ya nchi hivyo anastahiri pongezi na ndio maana nimeamua kumshirikisha katika single yangu,” alisema Linex.

Licha ya kutamba na ngoma hiyo, Linex alishawahi tamba na nyimbo zake kama, Mama Halima, Moyo wa Subira, Mrembo, Aifola aifola na nyinginezo ambazo zinafanya vizuri katika tasnia ya muziki nchini.

Saturday, September 15, 2012

ADHA ZA USAFIRI WAZIPATAZO WANAFUNZI WA TONGONI SEC SOCHOL

hapa wakiwa wanaelekea katika boti ilikuweza kuvuka baharii na kuweza kufika shuleni ambapo pana umbali wa kama kilometa 8 toka wavuke baharii
wakiwa wamekwisha karibia kupanda katika boti hiloo
hizi ndizo miundo mbinu wanazo tumia watoto wetu pindi wanapo taka kwenda shule pamoja na wakati wa kurudi kumbuka hapo kunawakati bahari hujaa kupita kiasi hivyo huwalazimu kutumia dakika 15 kusubiri mpaka maji yapungue kweli elimu ya tanzania inaitajika kuwezeshwa kwa hali na mali nadhani wadau wa elimu watakuwa wameliona hili na watalifanyia kazi


Tuesday, September 11, 2012

 WAANDISHI WA HABARI WAANDAMANA JIJINI DAR ES SALAAM, NI KUHUSU KIFO CHA DAUDI MWANGOSI
Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wahariri Bw. Neville Meena akizungumza mara baada ya waandishi wa habari kumaliza maadamano yao ya Amani kutoa ujumbe wao kwa jeshi la Polisi kutokana na kupoteza maisha kwa  mwandishi wa habari Marehemu Daudi Mwangosi aliyeuwawa katika vurugu kati ya Polisi na Wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika kijiji cha Nyololo Mkoani Iringa hivi karibuni, Maandamano hayo yalianzia katika ofisi za kituo cha Televisheni ya Chanel Ten ambako marehemu alikuwa mwakilishi wake mkoani Iringa na kuishia katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es salaam leo asubuhi.
Waandishi wa habari mbalimbali wakitoa dukuduku zao mara baada ya kumalizika kwa maandamano hayo leo asubuhi.
kweli sasa tumeamua hatutakli tena michongooo na polisii ona sasa mpaka tumeamua kufunga midomo na kalamu zetuu hatuna tena habari na polisiii dani ya siku40 hakuna kuandika habari zoozte zinazohusu polisi angalizo kwa wale makamanda wanaopenda kuuza katika vyombo vya habari
 hapa ni Waandishi wa habari wakiigiza vurugu zilizotokea  mkoani Iringa ambapo Mwandishi wa habari Marehemu Daudi Mwangosi alipoteza maisha katika vurugu hizo huo ni mfano jinsi jamama alivyoteswa na polisi dar kwelii alipata tabu marahemu.

Monday, September 10, 2012

chuda sasa mabingwa wapwa wa haniu cup mwaka 2012






Mgeni rasmi ambaye ni Mbunge wa viti Maalum Mkoa wa Tanga Amina Mwidau (CUF), akikabidhi zawadi ya kikombe cha ushindi kwa Nahodha wa timu ya Chuda FC Ibrahimu Bodwe, baada ya timu yake kuibuka kidedea katika michuano ya Haniu Cup, katikati ni Mratibu wa Mashindano hayo Mohammed Haniu.



HATIMAYE timu ya Chuda FC ya Chumbageni Jijini Tanga, imetwaa ubingwa wa mashindano ya Haniu Cup, kwa kuichapa kwa mikwaju ya penati timu ya Jiwe FC yenye maskani yake Tanga Sisi.
 Fainali hizo ambazo zilihudhuriwa na mamia ya wakazi wa Jiji la Tanga, zilikuwa za aina yake ambapo hadi kipyenga cha mwisho kinapulizwa timu hizo ziliweza kutoka sare ya bao 1-1.
 Chuda, ilifanikiwa kutwaa ubingwa wa mashindano hayo baada ya kuibuka na ushindi wa mikwaju ya penati 4 kwa 1 hali iliyowafanya mashabiki wa timu hiyo kutoka na shangwe uwanjani.
 Akizungumza katika mashindano hayo kabla ya kukabidhi zawadi kwa washindi hao Mbunge wa Viti maalum Mkoa wa Tanga, Amina Mwidau (CUF), alisema ni muhimu kwa mkoa huo kuwa na kiwanja mbacho kitakuwa ni mahususi kwa ajili ya kuibua vipaji wa soka mkoani humo.
 “Mimi kama Mbunge wetu wa Viti maalum na diwani wenu nina wajibu wa kusimamia kwa karibu shughuliza maendeleo ikiwemo kunua soka katika mkoa wetu huu wa Tanga. Mkoa huu ni chimbuko la michezo nchini na katika hili nitahakikisha ninawasilisha hoja katika kikao cha Jiji ili kuweza kijengwe kiwanja maalum ambacho itakuwa Soka Academy.

NA MWANDISHI  AHMAD NANDONDE.
                      
PWANI.

WAANDISHI WA HABARI NCHINI WAMETAKIWA KUANDIKA HABARI ZITAKAZOIBUA MIJADALA MBAYO ITAWAFANYA WANAUME KUSHIRIKISHWA KATIKA SUALA ZIMA  LA AFYA YA UZAZI WA MPANGO.

HAYO YAMESEMWA LEO DK.KATANTA SIMWANZA ALIPOKUWA AKIZUNGUMZA NA WAAANDISHI WA HAABRI KATIKA SEMINA  YA SIKU TATU INAYOFANYIKA MJINI BAGAMOYO.
DK.SIMWANZA AMESEMA ENDAPO MWANAUME ATASHIRIKISHA ATAWEZA KUTOA MCHANGO MKUBWA KATIKA JAMII HUSASANI SULA LA UZAZI WA MPANGO KUTOKANA NA UWEZO WA KUTOA MAAMUZI ALIONANO KATIKA JAMII NA HATA HALI YA KUJIAMINI.

AIDHA DK.KATANTA AMEWATAKA WATU KUTOKUWA NA DHANA INAYOAMINI KUWA WANAUME NI WAONEVU NA NI WATU WABAYA KWA JAMII NA KUWATAKA KUAACHANA NA DHANA HIYO KWANI WANAUME NI WAKISHIRIKISHWA WANAWEZA KULETA MABADILIKO KATIKA SUALA LA AFYA UZAZI WA MPANGO.

AKIZUNGUMZIA SUALA LA SERA YA AFYA BI.BEATRICE EZEKIEL AMEITAKA SERIKALI KUJIPANGA ILI KUFANIKISHA UTEKELEZAJI WA SERA YA JINSIA ILI KUWEZA KULETA MABADILIKO KATIKA JAMI NA HII NI KUTOKANA NA BAADHI YA HALMASHAURI KLATIKA DAWATI LA JINSIA LIMEKUWA LIKIKIKUMBWA NA CHANGAMOTO ZITOKANAZO NA UKOSEFU WA VITENDEA KAZI NA FEDHA.

AMEONGEZA KUWA ILI KUTEKELEZA SERA NI LAZIMA SREKILALI KKUTENGA KIASI CHA FEDHA IKIWA NI PAMOJA NA KUWA UTARATIBU WA KUWAWEZESHA WANAHABARI KUPATA TAARIFA SAHIHI NA KWA KAWATI ILI WAWEZE KUFIKISHA TAARIFA KWA  JAMII HUSIKA.

HATA HIVYO KWA UPANDE WAKE MWEZESHAJI  MWENGINE KATIKA SEMINA HIYO BW. SOSPETER  MAGUMBA  AMESEMA TATIZO LA JINSI LIMEKUWA LIKIWAELEMEA ZAIDI WANAUME KUTOKANA NA KUJIHUSISHA NA MAMBO MENGI YA KUISAIDAIA FAMILI HALI INAYOMFANYAKUSHINDWA KUSHIRIKI IPASAVYO KATIKA SUALA ZIMA LA UPANGAJI WA UZAZI WA MPANGO.

SEMINA HIYO IMEEANDALIWA NA SHIRIKA LA KIMATAIFA LA NCHINI UJERUMANI LA GIZ KWA LENGO LA KUELIMISHA WAANDISHI WA HABARI MASUALA MBALI MBALI YA JINSI JINSIA NA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI.

WANAHABAR WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA WAKIPASHA MWILI NA WAWEZESHAJI WAO BAADA YA KIKAO CHA MUDA MREFU 
Rahabu fungo fred mtangazaji wa radio free afrika pia ni mke wa mtangazaji machachari fred fidelis au fredwaa akichangia jambo katika semina hiyo.
Wakiwa katika semiana ya siku tatu iliyomalizika leo bagamoyo millenium hotel ikihusisha wanahabar na watu wa shirika la GIZ kwa lengo la la kuhamasisha wanahabari kuandika habari zinazohusu masuala ya jinsia na maambukizi ya virusi vya ukimwi kutoka kulia ni kwanza kulia ni mwezeshaji kutoka shirika la ujerumani la giz mama beatrice ezekiel anayefuata ni mwandishi na mtangazaji wa radio victoria fm musoma bw. ahmad jay nandonde ,james mbuligwe kutoka wananchi blog na mwisho ni mtangazaji wa radio jamii ya wamasai mkoani manyara bw jackson 


Thursday, September 6, 2012

Mwandosya, Slaa sasa wamua kugawana’ watoto wa hayati Mwangosi

Mjane wa Daudi Mwangosi aliyekuwa mwandishi wa Channel Ten,Itika akilia kwa uchungu juu ya kaburi la mumewe kwenye mazishi yaliyofanyika kijijini kwake Kasoka wilayani Rungwe mkoani Mbeya jana.Picha kwa hisani ya kikwatojr.blogspot.com

MAZISHI ya Mwandishi wa Habari, Daud Mwangosi yalifanyika jana katika Kijiji cha Busoka kilichoko wilayani Rungwe, Mbeya na kuhudhuriwa na mamia ya waombolezaji wakiongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa. Katika mazishi hayo, viongozi hao wawili kila mmoja alitangaza kuwasomesha watoto wa marehemu Mwangosi ambaye alifariki dunia Septemba 2, mwaka huu baada ya kupigwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu wakati polisi walipokuwa wakisambaratisha mkutano wa Chadema.


Akitoa salamu zake katika mazishi hayo, Profesa Mwandosya alisema yupo tayari kumsomesha mtoto wa kwanza kati ya wanne wa Mwangosi, Nehemia ambaye anasoma kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Malangali.

Alisema atamsomesha mtoto huyo kidato cha tano na sita na ikiwa atafaulu na kukosa mkopo wa elimu ya juu, atamsomesha mpaka atakapomaliza elimu yake ya juu.

Dk Slaa kwa upande wake, alisema amewasiliana na rafiki yake ambaye yupo tayari kuwasomesha watoto wawili wa Mwangosi ambao wote wapo shule ya msingi. Mtoto wa mwisho wa marehemu hajaanza masomo.
Pamoja na kuwasomesha watoto hao, alisema Chadema kimetoa Sh2 milioni za rambirambi kutokana na msiba huo.

Vijembe msibani
Awali, Profesa Mwandosya na Dk Slaa walitoa kauli zinazoonyesha kupigana vijembe vya kisiasa, baada ya waziri huyo kumtaka Dk Slaa aache kufanya kampeni za kuingia Ikulu mwaka 2015 msibani.

Kauli hiyo ya Profesa Mwandosya ilikuja baada ya Dk Slaa kutaka polisi waliohusika na mauaji hayo wachukuliwe hatua za kisheria kwa sababu wanajulikana.

“Tunashangaa wamekamatwa watu wengine na kuwaacha waliohusika na mauaji hayo, tunawajua kwa sababu wameonekana hadharani, hakuna siri kwa hilo,” alisema Dk Slaa.

Akizungumza baada ya kauli hiyo ya Dk Slaa, Profesa Mwandosya aliwataka wanasiasa wa vyama vya upinzani kuacha kutumia misiba kutafuta kura za urais mwaka 2015.

“Natoa pole sana kwa familia na tasnia nzima ya habari nchini. Hiki ni kipindi kigumu, lakini tuviachie vyombo husika vifanye uchunguzi wa mauaji haya,” alisema Profesa Mwandosya na kuongeza:
“Lakini nichukue fursa hii kuwaomba wanasiasa waache kutumia misiba ili kujipatia umaarufu katika kutafuta kura za urais mwaka 2015.”

Katika mahubiri yake msibani hapo, Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Busoka, Mathayo Mwanjemele alikemea mauaji hayo na kuwaomba wahusika wajitokeze hadharani kabla Mungu hajawaumbua.

“Waliohusika na mauaji haya wajitokeze na kutubu kwa wananchi kabla adhabu ya Mungu haijawakuta,” alisema.

Alisema ufike wakati Serikali iwe inakiri uzembe unaofanywa na watendaji wake ambao umekuwa ukitokea mara kadhaa.

       kwaupende wa IGP Mwema asimamia uchunguzi ni haki?
Kabla ya mazishi hayo, mwili wa Mwangosi ulifanyiwa uchunguzi na wataalamu wa afya kutoka Dar es Salaam, huku IGP Said Mwema akishuhudia.

Baada ya kumalizika uchunguzi huo, usiku mwili wa marehemu ulisafirishwa kuelekea Mbeya kwa mazishi.

Mwili huo ulipofika Tukuyu, umati mkubwa ulijipanga barabarani na kupunga mkono, huku wengine wakiusindikiza kwa baiskeli na pikipiki hadi kijijini, Busoka.

          Majeruhi wengine 
Akizungumzia tukio hilo, Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mafinga, Dk Peter Mwenda alisema mbali na marehemu Mwangosi, watu wengine 10 walijeruhiwa, wawili kati yao walitibiwa na kuruhusiwa. Alisema waliobaki hospitalini hapo hali zao zinaendelea vizuri.

Aliwataja majeruhi hao kuwa ni Hussein Kweha (27), Edson Iddy (22), Alfred Kibitanyi (27), Hamad Musa (37), Yeremia Kulwa (45) na Christopher Pesa (30).

Alisema majeruhi hao walidai kwamba walikuwa katika mkutano wa ndani wa Chadema na askari waliwataka kutulia kabla ya kuwashambulia kwa marungu na vitu vyenye ncha kali.
 
 shukuranii za pekee kwa blog hii kwa kuzidi kufatilia kila walatii ewee usomaji wanguu . kutoka kwa kikwatojr
Powered by Blogger.