Blogger Widgets 2013 | Mfaume Kikwato JR

PALACE HOTEL

PALACE HOTEL

Vumbua Hazina chini ya kizibo

Vumbua Hazina chini ya kizibo
+255788788218

BAYPORT

BAYPORT
KOPA BAYPORT

Saturday, September 14, 2013

MAMA MANGWEA AJITOSA KUMTETEA MWANA FA...!!

Mama wa MwanaHip Hop aliyewahi kuaminika kuwa bingwa wa mitindo huru, Albert Mangwea aliyefariki mwezi Mei mwaka huu, Denisia Costantine Mangwea ameibuka na kumtetea mwanamuziki wa kizazi kipya Hamis Mwin’juma ambaye anatuhumiwa kuahidi pesa kwa mama huyo na kuingia mitini.


  
Sakata hilo ambalo limekuwa likiripotiwa tangu mwishoni mwa wiki iliyopita, linatokana na kitendo cha mwanamuziki huyo (MwanaFA) ambaye aliwahi kuahirisha onesho lake, baada ya kifo cha msanii mwenzake (Albert Mangwea), kutokuweka hadharani hitimisho la ahadi aliyoitoa kwa familia ya marehemu.
Tarehe 31 ya mwaka huu ilikuwa ni tarehe ya onesho la The Finest ambalo MwanaFA alikuwa akitimiza miaka 13 ya muziki wake, akawa na lengo pia na kuugeuza muziki wa Hip Hop uwe na sura ya kistaarabu na kibiashara pia ili kuuongezea aina ya mashabiki.
Siku moja kabla ya onesho, msiba wa Albert Mangwea ukatokea, na hapo ikamlazimu mwanamuziki huyo kuahirisha onesho lake, na kulisogeza wiki mbili mbele huku akiahidi asilimia 15 ya faida atakayopata, angeipeleka kwa familia ya Albert Mangwea.
Baada ya mazishi, Onesho la The Finest lilifanyika Juni 14, na baada ya hapo, MwanaFA hakuonekana akisema kwenye mitandao wala kwenye redio kuhusiana na mapato yake kwenye onesho hilo na kiasi gani alipeleka kwa Mama Mangwea. Tangu onesho hilo, huu ni mwezi wa tatu na ndipo gazeti moja la kila wiki likaandika kuhusiana na suala hilo, jambo ambalo linaendelea kuzungumzwa kila kukicha kwenye vyombo vya habari. Na ndipo gazeti hili liliamua kwanza kumtafuta Mwana FA na kuongea naye.
Kauli ya MwanaFA
Akiongea na Mwananchi, MwanaFA alikiri kuahidi kutoa fedha hizo na aliahidi asilimia 15 ya faida  itakayotokana na mapato ya onesho la The Finest.
“Nakiri kukosea jambo moja, nilipoahidi, niliongea na wanahabari lakini wakati wa kutoa, nilitoa bila kutangaza, na hii kutoa jamani ni moyo, haina haja kumtangaza mtu kwa kuwa umemsaidia au umempa pole”, alifafanua MwanaFA
Alisema katika mapato aliyoyapata kutokana na onesho hilo ambayo yalikuwa ni jumla ya shilingi 19.5 milioni, alitoa milioni tatu na kuzikabidhi kwa mama huyo, ingawa si taslimu, aliziingiza kwenye akaunti yake, katika benki ya Exim. Alifafanua kwamba alilifanya hili kwa moyo na hakuwa na nia ya  kujitangaza kwa hiyo alilimaliza akawa anaendelea na shughuli zake. Baada ya kauli hii, Mwananchi likapiga mguu mpaka Kihonda kwa mama yake Mangwea, Bi Denisia Costantine Mangwea
Mama Mangwea ashangaa!
Alipoulizwa kuhusiana na sakata hilo Mama Mangwea alikiri kwamba ameumia sana moyo baada ya kusikia ripoti ya kwamba MwanaFA anadaiwa hakutoa hizo pesa kwani alitoa kipindi kile kile cha msiba.
Kabla hata ya arobaini, aliweka benki kisha akaja na mwenyewe, hakuna na waandishi kama wanavyofanya wenzake, alikuja mwenyewe tukaongea, na mara kwa mara tunawasiliana, wanataka kumtia doa kijana wa watu ni muungwana sana”, alifafanua mama Mangwea.

MTUHUMIWA WA UBAKAJI AHENYESHA POLISI...



KATIKA hali isiyo ya kawaida, kijana Faizi Haji Juma (22), mkazi wa Mchanga wa Kwale Wilaya ya Chakechake, Pemba aliwashangaza wananchi baada ya kuwatoroka askari waliokuwa wamemdhibiti ndani ya jengo la mahakama ya wilaya hiyo.
Kijana huyo anayekabiliwa na makosa mawili katika mahakama mbili tofauti, likiwemo la ubakaji na shambulio la mwili kwa lengo la kutaka kubaka, aliwachomoka askari na kukimbilia baharini katika Soko la Katari.
Baada ya kukimbia kwa muda, askari wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba, Agustino Awe na Koplo Mohamed Hamza, walilazimika kumkimbiza kwenye matope na kuhakikisha wanamtia mikononi mtuhumiwa huyo na kumrudisha mahakamani.
Baada ya kurudishwa ndani ya viunga vya mahakama ya wilaya, mtuhumiwa huyo alitakiwa kuieleza korti sababu zilizomfanya akimbie lakini akaishia kubabaika.
Hakimu Omar Mcha Hamza alihamaki baada ya kushuhudia tukio hilo ambapo aliporejeshwa, aliamuru mtuhumiwa huyo kurudishwa rumande.



PICHA:RAIS SHEIN AMTEMBELEA PADRI ALIYEMWAGIWA TINDIKALI MJINI UNGUJA..




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Padri Joseph Monesmo Magamba, wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui, alipofika katika Hospitali ya Mnazi Mmoja kumpa pole,Mjini Unguja,baada ya kumwagiwa tindikali na watu wasiojulikana katika Mtaa wa Mlandege Mkoa wa Mjini Magharibi jana jioni, Padri alimwagiwa Tindikali alipokuwa akitoka kupata huduma ya Mtandao 
 
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akimsikiliza Padri Joseph Monesmo Magamba,wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui,akitoa maelezo jinsi alivyopata mkasa wa kutiwa  Tindikali jana na watu wasiojulikanwa,katika mtaa wa Mlandege Mjini Unguja, alipofika katika Hospitali ya Mnazi Mmoja kumpa pole,ambapo amelazwa na kuapatiwa matibabu.
 
 
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiwafariji jamaa  na ndugu wa Padri Joseph Monesmo Magamba,wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui,waliofika katika Hospitali ya Mnazi Mmoja kumpa pole Padri huyo baada ya kumwagiwa Tindikali na Watu wasiojulikanwa jana jioni Mtaa waMlandege Mjni
 
 Mmoja wa Ngugu wa Padri Joseph Monesmo Magamba,wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui,akimueleza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,hisia zake kwa Uchungu kutokana na kitendo hicho cha kumwagiwa Tindikali na watu wasiojulikanwa  kwamba zilichukuliwe hatua za kisheria na kukomeshwa Vitendo kama hivyo
 
 
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akifafanua jambo wakati akiwafariji jamaa na ndugu wa Padri Joseph Monesmo Magamba,wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Machui,waliofika kumuangalia Padri huyo aliyelazwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja baada ya kumwagiwa Tindikali na Watu wasijulikanwa jana jioni katika Mtaa wa Mlandege Mjini Unguja

Thursday, August 8, 2013

MBUNGE wa kuteuliwa, James Mbatia (NCCR-Mageuzi), ameibua madudu mapya katika sekta ya elimu

MBUNGE wa kuteuliwa, James Mbatia (NCCR-Mageuzi), ameibua madudu mapya katika sekta ya elimu, ambao umebaini kwamba kwenye mitihani ya majaribio ya darasa la saba, baadhi ya maswali ya kuchagua, hayakuwa na majibu.

Mitihani hiyo ya majaribio ya programu maalum ya matokeo makubwa sasa, kwa mujibu wa Mbatia ilifanywa na wanafunzi wa darasa la saba hivi karibuni katika masomo ya Hisabati, Kiswahili na Kiingereza katika wilaya 40 nchini.

Katika uozo huo ambao ameutaja kama kuwakatisha tamaa wanafunzi katika somo la Hisabati, Mbatia alisema maswali sita yalibainishwa na wataalamu wa Hesabu kuwa hayana majibu huku swali moja likiwashinda maprofesa waliofanya mtihani huo.

Alisema katika swali moja, namba 33 walimu wa hisabati katika shule kubwa za msingi walishindwa kulifanya na baadaye kubainika kuwa ni swali la mwanafunzi anayechukua fani ya uhandisi katika vyuo vya elimu ya juu.

Mabatia alisema katika mitihani hiyo, kunamakosa mbalimbali ya lugha pamoja na usahihi wa masuala mbalimbali, ikiwemo programu hiyo kuainishwa kama matokeo makubwa sasa huku jina la wizara likiandikwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi.

Alisema katika mtihani huo wa hisabati,ambao wanafunzi wa darasa la saba walitakiwa kufanya kwa saa mbili, mtaalamu wa aligebra aliufanya kwa saa 2:10 na profesa saa 2:03 huku yeye akifanya kwa saa 2:19.

“Matokeo haya ni kuwakatisha tamaa na kuwaua wanafunzi kabla ya kufanya mitihani, ni lazima hatua madhubuti zichukuliwe kuokoa mapigo haya ya moyo wa Taifa ambayo yakizimika, Taifa linakufa,” alisema.

Mbatia alitoa mapendekezo yake ili kuokoa janga hili la elimu ikiwa ni pamoja na kuundwa kwa Tume ya Kudumu ya Elimu, itakayoshughulikia kuhakikisha ubora wa elimu nchini. Tume hiyo kwa mujibu wa Mbatia, inatakiwa kuwa na mamlaka ya kuhakiki utendaji wa taasisi mbalimbali za elimu, ambazo hadi sasa zimeonekana kutotimiza vyema wajibu wake.

“Ninaamini kwamba,tume hiyo itakapoundwa itasaidia kubainisha wazi nini falsafa na malengo hasa ya utoaji wa elimu nchini, kulingana na wakati tulionao, jambo ambalo halitakuwa geni kwani katika uongozi wa awamu ya kwanza, kulitungwa falsafa na miongozo mbalimbali,”alisema

Alisema kwa mamlaka aliyonayo Rais na na kwa mujibu wa katiba na kwa kadri anavyoona inafaa, anaweza kuunda tume na kuipatia majukumu ya utendaji stahiki, ikiwemo kutoa idhini ya matumizi ya mitaala mingine.

Pia alipendekeza tume hiyo ihariri na kupitia vitabu vya kiada kwa shule nchini na kufanya utafiti za kisayansi kuhusu masuala mbalimbali ya elimu kwa lengo la kuinua ubora wa elimu.

Akizungumza na Blog hii , Msemaji wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Bunyanzu Ntambi alikiri kuwa jinala wizara limekosewa katika mitihani hiyo. Alipoulizwa kuhusu uozo uliopo katika mitihani hiyo ya majaribio, alisema atafuatilia na atatoa taarifa kwa gazeti hili baadaye.

Wednesday, August 7, 2013

WAZAZI WAKATAZA WALIMU WASIWAFUNDISHE WATOTO WAO JINSI YA KUTUMIA CONDOM

Imeelezwa kuwa Baadhi ya wazazi na walezi wilayani Kahama mkoani Shinyanga wamekuwa wakiwazuia walimu kutoa elimu ya njia ya kujikinga na ukimwi kwa watoto wao wa sule za msingi ikiwemo matumizi sahihi ya condom. 

Hayo yamebainika leo katika semina iliyoandaliwa na shirika la UNESCO iliyojumisha wakuu wa shule za msingi na sekondari pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali iliyofanyika katika ukumbi wa Golden Valley Mjini Kahama.

Akichangia hoja katika semina hiyo Mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Korogwe Bi Ashura Rugakingira amesema kuwa wamekutana na tatizo hilo toka kwa baadhi wazazi hao licha ya kuwa somo hilo lipo katika mtaala wa Serikali.

Rugakingira amesema kuwa changamoto hiyo inawafanya walimu wengi kukata tamaa ya kutoa elimu hiyo ya kupambana na maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa wanafunzi hao.

Awali akifungua semina hiyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu Bi Isabela Chilumba amewataka walimu hao kuvunja ukimya na kuwa wawazi kuzungumza na wanafunzi wao kuhusu Maambukizi ya virusi vya ukimwi na UKIMWI.

Sambamba na hayo Chilumba ametoa angalizo kwa wananchi kutodanganyika na takwimu za maandishi zinazotolewa na kwamba kila mtu awe mstari wa mbele kupima afya yake mwenyewe.

Naye Msimamizi wa mradi huo wa Elimu ya Afya ya UKIMWI, uzazi na maadili kwa vijana kutoka UNESCO Mathius Herman amesema lengo la mradi huo ni kujenga mahusiano rasmi kati ya Mashirika yasiyo ya serikali na shule.

Tuesday, July 16, 2013

UTAFITI: WANAUME HUVUTIWA ZAIDI NA SURA WANAPOTAFUTA MKE LAKINI HUVUTIWA NA UMBO WANAPOTAFUTA MWANAMKE WA "KUCHEZEA"




hili ni jambo la kuchunguza sana na lakulifatilia kwa umakini zaidi ili usije ukafanya kama hivi na wewee

  • Mabinti: Siri imeshafichuka na inavyoonekana wanasayansi tayari wameshafumbua lile fumbo tata la nani mwoaji na nani mbabaishaji tu mtaka uroda.
  • Siku nyingine mpenziyo mpya akikuambia kwamba sababu yake kuu ya kukupenda ni miguu yako, macho, kiuno, matiti, umbo namba nane au sababu zingine za kiumbo, kuna uwezekano mkubwa kwamba huyo njemba si mwoaji bali ni mtafuta uroda tu.
  • Utafiti mpya uliofanywa katika Chuo Kikuu cha Texas, Austin unaonyesha kwamba wanaume hutumia vigezo tofauti wanapotafuta mwenzi.
  • Kama lengo ni kutafuta mwenzi wa kudumu (mf. mke) basi wanaume wengi hupendelea wanawake wenye sura nzuri lakini kama lengo ni uhusiano wa muda mfupi tu (mf. kutimiza tamaa za ngono za muda mfupi) basi wanaume wengi hutafuta wanawake wenye maumbo mazuri wayatamaniyo
     
    Watafiti hawa wamegundua kwamba, japo umbo ni muhimu kidogo katika mahusiano ya muda mrefu, uso ni muhimu zaidi kwa sababu ndicho kiashiria kizuri cha umri na “rutuba” ya mwanamke.

Monday, July 15, 2013

BINTI ABAKWA MPAKA KUFA MBELE YA NYUMBA YA IBADA

Binti mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Mariam umemkuta umauti baada ya kubakwa mpaka kufa,vijana hao waliokosa utu na kushindwa kumuogopa Mungu walifanya kitendo hicho mbele ya eneo la kanisa huko Nachingwea Lindi.Marehemu akitoka Nachingwea Resort  katika muziki siku ya ijumaa.Inasadikika kuwa marehemu alikuwa amelewa na watu walio mbaka alitoka nao kwenye muziki.


Emungu tunusuru na hili kadhia mana tunakoelekea kwa sasa siko jamani tubadilike

CHAMA CHA TIBA ZA ASILI(ATME) WABARIKI MATUMIZI YA MAFUTA YA UBUYU, WASEMA HAYANA MADHARA YOYOTE KWA AFYA YA BINADAMU...!!

Sasa ni kati ya Chama cha Tiba Asili (ATME) na  TDFA.  ATME kinadai hayana madhara wagonjwa wake wameyatumia kwa zaidi ya miaka 20.
Dar es Salaam. Mratibu wa Chama cha Watabibu wa Dawa za Asili Tanzania (ATME), Boniventure Mwalongo amesema taarifa zilizotolewa hivi karibuni na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TDFA) kuhusu matumizi ya mafuta ya ubuyu zinaweza kuleta madhara kwa jamii kwa sababu watu wengi wamekuwa wakiyatumia.
Akitolea mfano watumiaji wakubwa  wa mafuta hayo, Mwalongo alisema, wenye magonjwa kama ya moyo na wanaoishi na Virusi vya Ukimwi wamekuwa wakiyatumia mafuta hayo kwa muda mrefu na kudai yamewasaidia.
Mwalongo ameyasema hayo jana baada ya hivi karibuni kuibuka utata kuhusu ubora na usalama wa mafuta hayo na kudai kuwa wao kama ATME walianza kuyatumia kama dawa kwa wateja wao siku nyingi na hawajawahi kupata malalamiko yoyote na kuwahakikishia watumiaji kuwa hayana madhara.
 
 
 
 
 Yametumika kwa zaidi ya miaka 20 na sisi tunazo kumbukumbu za wagonjwa tuliowapa mafuta hayo kama dawa na hatujawahi kupata ripoti yoyote ya madhara kwa wale waliotumia,” alisema Mwalongo.   TFDA ilitoa taarifa kwamba mafuta hayo hayafai kwa matumizi ya binadamu kwa sababu yana kiwango kikubwa cha tindikali ya mafuta aina ya cyclopropenoic fatty acids.

  Katika taarifa ya TFDA iliyotolewa juma lililopita ilisema athari zinazoweza kutokea kutokana na matumizi ya mafuta hayo ni pamoja na kuathiri vimeng’enyo vinavyosaidia katika uchakataji wa tindikali za mafuta mwilini.
  Pia ilisema ili yaweze kukidhi vigezo vya ubora na usalama ni lazima yafanyiwe usafishaji wakati wa usindikaji na kwamba kwa sasa nchini hakuna aina ya usindikaji unaofanyika wenye uwezo wa kuondoa tindikali hiyo ya cyclopropenoic fatty acids katika mafuta ya mbegu za ubuyu.
 Hata hivyo Mwalongo alikemea usambazaji holela wa mafuta hayo hasa baada ya kubainika kuwa yanatibu maradhi mbalimbali ambapo baadhi ya wajasiriamali wamekuwa wakiyasambaza wakati siyo wataalamu wa tiba asili.
  Mratibu huyo alizishauri mamlaka zinazohusika na suala zima la afya ya binadamu nchini kutoa majibu yatakayosaidia kuondoa mgawanyiko uliopo sasa kutokana na mafuta hayo badala ya kutoa taarifa za kutisha.
   Hata hivyo alipoulizwa Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Tiba Asili kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Paul Mhame, alisema hawana taarifa zozote kama kuna tafiti zimefanyika kuhusiana na matumizi ya mafuta hayo.

.MACHANGUDOA DAR WASEMA "MCHANA TUNAFUNGA, USIKU TUNAJIUZA TUPATE HELA YA FUTARI NA DAKU"....

OPARESHENI Fichua Maovu (OFM) inayoendeshwa na mapaparazi wa Global Publishers inazidi kufichua ‘madudu’ kwenye jamii, safari hii imekutana na machangu ambao wamecharuka kuendeleza biashara hiyo kwa kisingizio cha kutafuta fedha za kununulia futari.


‘Askari’ wa OFM, wiki iliyopita alifanya uchunguzi katika viunga mbalimbali maarufu kwa biashara hiyo na kukuta machangudoa wakifanya biashara yao kama inavyokuwa katika miezi ya kawaida.
Maeneo ambayo yalionekana kushamiri zaidi kwa biashara hiyo ni Barabara ya Mwananyamala Hospitali, American Chipsi, Makaburi ya Kinondoni, Viwanja vya Leaders Club, Taasisi ya Moyo, Jolly Club (Masaki), Hospitali ya Agha-Khan, New Maisha Club (Masaki) na Coco Beach.

Saturday, February 23, 2013

matokeo kidato cha nne wawili wajiua, wawili wanusurika

KUFUATIA kupata matokeo mabaya ya matokeo yao ya kidato cha nne yaliyotangazwa wiki iliyopita jumla ya wahitimu wawili tayari wameshapoteza maisha kwa kujinyonga huku wawili wakiwa wameokolewa wakiwa katika harakati za kujiua 

Kati ya waliojinyonga ni Barnaba Venant [18] mkazi wa Mbagala ambaye alihitimu katika shule ya Sekondari ya Debrabant Mbagala ya jijini Dar es Salaam Akielezea tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Englibert Kiyondo, alisema tukio hilo lilitokea juzi, majira ya saa 4 asubuhi huko maeneo ya Nzasa, Mbagala

Amefafanua kuwa, marehemu huyo alichukua uamuzi huo baada ya kutoridhishwa na matokeo yake ya mtihani wa kidato cha nne ambayo yalibainishwa alipata daraja la nne point 27 kinyume na matarajio yake

Amesema kijana huyo alijinyonga kwa kutumia kamba ya manila, aliyokuwa ameitundika kwenye dari ndani ya stoo ya nyumba yao. Katika tukio lingine la aina hiyo, Michael Fidelis[19] aliyehitimu Shule ya Sekondari ya Kanyenye mjini Tabora

Imedaiwa kuwa, mhitimu huyo alipogundua amepata daraja sifuri aliporudi nyumbani alichukua maamuzi ya kujinyonga hadi kufa akiwa chumbani kwake kwa kutumia kamba ya manila.

Na kuacha ujumbe uliosomeka “Mama usitafute mchawi, uamuzi niliouchukua ni sababu ya matokeo yangu mabaya, nakutakia maisha mema, nisamehe sana mama.”

Kufuatia matokeo hayo mabaya yaliyoleta historia vijana wengine wawili mmoja mkazi wa Kimara Temboni jijini Dar es salaam amenusurika kutoa uhai wake kwa kutoridhishwa na matokeo hayo

Mwingine aliyefahamika wka jina la Hoseph Hoseah [18] mkazi wa mkoani Pwani alikimbizwa zahanati akwia aktika jaribio la kutoa uhai wake baada ya matokeo yake kuonyesha amepata daraja la nne jambo ambalo lilimfanya asiwe na raha tokea apokee matokeo hayo

Imedaiwa na mmoja wa ndugu wa kijana huyo kuwa ndugu yao huyo alikuwa ni mmoja kati ya wanafunzi watano ambao shule ilikuwa ikiwatarajia wataleta sifa kwa kuleta daraja la kwanza shuleni hapo

Matokeo yaliyotangazwa mwanzoni mwa wiki hii na Waziri wa Elimu yanaendelea kuleta migogoro kwa wadau huku waziri huyo akitakiwa kujiuzuru

msanii Ragga Dee adondosha kichupa kipya

Akiwa ni msanii mwenye nidhamu na heshima katika kazi yake kiasi cha kupata heshima kubwa kutoka kwa mashabiki na wadau wa muziki nchini Uganda, msanii Ragga Dee adondosha kichupa kipya alichokibatiza jina 'Katonda Kyasalawo'

Ragga Dee ameelezea kuwa hivi sasa anaongeza nguvu akijikita zaidi katika miondoko ya Zouk na Soukous akitumia sana lugha ya kiLuganda, kiingereza na Lingala.
kicheki kichupa chake kipwa hapa 

ideaja na ujio mpya na mzee mzima Prof Jay

Baada ya miaka mingi kupita tangu gwiji wa miondoko ya Hip Hop na Bongofleva, Joseph Haule  aka Prof. Jay kufanya kolabo na mwanashosti Judith Wambura aka Lady Jaydee, hatimaye wawili hao wamefungua mwaka kwa kuwapa mashabiki habari njema juu ya ujio wao wa pamoja.

Profesa Jay ameonyesha fuaraha yake hiyo kutokana na wawili hao kuiteka tasnia hii ya muziki kwa miaka mingi ambapo pia mwanashosti Jay Dee anatarajia kurekodi albamu yake mpya itakayokuwa ni ya sita kutoka kwa mwaka huu.

Saturday, February 2, 2013

Sugu aiponda Bongoflava



 Mr 2 a.k.a Sugu jamaa aliyeanza muziki kitambo sana na ambaye siku hizi pia ni mbunge wa jimbo la Mbeya mjini kwa jina halisi anajulikana kama Joseph Mbilinyi, aliwaponda wasanii wa bongoflava kwa kuongelea vitu visivyokuwepo.
 
“Mi mara nyingi huwa sisikilizi muziki wa bongoflava maana hawaimbi mambo yanayotokea sasa katika jamii wala mambo yanayoigusa jamii. Kuna mambo mengi sana ambayo unaweza ukaimba na ukaigusa jamii, sio kila siku kuimba nyimbo za aina zisizoeleweka hata jamii inashindwa kukuelwa”. Alisema Sugu.
 
Kuliko kusikiliza muziki wa bongoflava Mr Sugu alisema ni heri kumsikiliza msanii Koffi  Olomide wa Kongo maana nyimbo zake japo ni za kucheza ila zina ujumbe unaoendana na jamii ya leo na hata unapousikiliza masikioni hauchoshi mapema.

Watanashati Yaboreshwa Zaidi

NewsImages/6787526.jpg   
Kampuni ya Mtanashati Entertainment inayo milikiwa na Ostazi Juma namusoma, inayojihusisha na burudani, sasa imeboreshwa zaidi na kuaza kutengeneza Nguo mbalambali zikiwemo za watoto
 kampuni ya Mtanashati Entertaiment yenye makazi yake maeneo ya Magomeni Mapipa mtaa wa Idirisa jijini Dar es salaam, imeaza kutengeneza mavazi mbalimbali yakiwemo ya watoto.

Kampuni ya Mtanashati Entertainment imeudhihirishiwa watanzania kuwa ipo kikazi zaidi, baada ya baada ya kuwanzisha utengenezaji wa nguo na vifaa mbalimbali kama vile miganda na mabegi.

kampuni hiyo, ambayo inamiliki wasanii wa bongo flava waonaofanya vizuri kwa sasa katika anga ya muziki wa Tanzania, miongoni mwa wasanii waliyopo chini ya kampuni hiyo, ni P.N.C, Dogo Janja, J FIL DAV, HAPPY BALICE NA AMAZON.

Msanii P.N.C kwa sasa anatamba na wimbo wake imebuma huku msanii Dogo janja ameonesha kuwatishia wasanii wengi wakubwa baada ya kujiunga katika kundi hilo na kutoa singo yake aliyomshirikisha msanii mwenzake P.N.C katika Single yake mpya inayokwenda kwajina la Ya moyoni.

Kampuni hiyo ilianzishwa 19/2009 na kuzinduliwa rasmi tarehe 9/9/2012 ndani ya Clab Bilcanas, toka kuzinduliwa kwa kampuni imeleta mapinduzi makubwa katika mziki wa Tanzania

Thursday, January 10, 2013

hayo ni ya huko musoma

Mratibu wa shughuli za bima ya afya MUSOMA Dk.Gideon Mkingira  ambaye pia ni mgeni rasmi katika warsha hiyo akizungumza jambo(picha na ahmad nandonde)musoma


Powered by Blogger.