Blogger Widgets July 2013 | Mfaume Kikwato JR

PALACE HOTEL

PALACE HOTEL

Vumbua Hazina chini ya kizibo

Vumbua Hazina chini ya kizibo
+255788788218

BAYPORT

BAYPORT
KOPA BAYPORT

Tuesday, July 16, 2013

UTAFITI: WANAUME HUVUTIWA ZAIDI NA SURA WANAPOTAFUTA MKE LAKINI HUVUTIWA NA UMBO WANAPOTAFUTA MWANAMKE WA "KUCHEZEA"




hili ni jambo la kuchunguza sana na lakulifatilia kwa umakini zaidi ili usije ukafanya kama hivi na wewee

  • Mabinti: Siri imeshafichuka na inavyoonekana wanasayansi tayari wameshafumbua lile fumbo tata la nani mwoaji na nani mbabaishaji tu mtaka uroda.
  • Siku nyingine mpenziyo mpya akikuambia kwamba sababu yake kuu ya kukupenda ni miguu yako, macho, kiuno, matiti, umbo namba nane au sababu zingine za kiumbo, kuna uwezekano mkubwa kwamba huyo njemba si mwoaji bali ni mtafuta uroda tu.
  • Utafiti mpya uliofanywa katika Chuo Kikuu cha Texas, Austin unaonyesha kwamba wanaume hutumia vigezo tofauti wanapotafuta mwenzi.
  • Kama lengo ni kutafuta mwenzi wa kudumu (mf. mke) basi wanaume wengi hupendelea wanawake wenye sura nzuri lakini kama lengo ni uhusiano wa muda mfupi tu (mf. kutimiza tamaa za ngono za muda mfupi) basi wanaume wengi hutafuta wanawake wenye maumbo mazuri wayatamaniyo
     
    Watafiti hawa wamegundua kwamba, japo umbo ni muhimu kidogo katika mahusiano ya muda mrefu, uso ni muhimu zaidi kwa sababu ndicho kiashiria kizuri cha umri na “rutuba” ya mwanamke.

Monday, July 15, 2013

BINTI ABAKWA MPAKA KUFA MBELE YA NYUMBA YA IBADA

Binti mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Mariam umemkuta umauti baada ya kubakwa mpaka kufa,vijana hao waliokosa utu na kushindwa kumuogopa Mungu walifanya kitendo hicho mbele ya eneo la kanisa huko Nachingwea Lindi.Marehemu akitoka Nachingwea Resort  katika muziki siku ya ijumaa.Inasadikika kuwa marehemu alikuwa amelewa na watu walio mbaka alitoka nao kwenye muziki.


Emungu tunusuru na hili kadhia mana tunakoelekea kwa sasa siko jamani tubadilike

CHAMA CHA TIBA ZA ASILI(ATME) WABARIKI MATUMIZI YA MAFUTA YA UBUYU, WASEMA HAYANA MADHARA YOYOTE KWA AFYA YA BINADAMU...!!

Sasa ni kati ya Chama cha Tiba Asili (ATME) na  TDFA.  ATME kinadai hayana madhara wagonjwa wake wameyatumia kwa zaidi ya miaka 20.
Dar es Salaam. Mratibu wa Chama cha Watabibu wa Dawa za Asili Tanzania (ATME), Boniventure Mwalongo amesema taarifa zilizotolewa hivi karibuni na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TDFA) kuhusu matumizi ya mafuta ya ubuyu zinaweza kuleta madhara kwa jamii kwa sababu watu wengi wamekuwa wakiyatumia.
Akitolea mfano watumiaji wakubwa  wa mafuta hayo, Mwalongo alisema, wenye magonjwa kama ya moyo na wanaoishi na Virusi vya Ukimwi wamekuwa wakiyatumia mafuta hayo kwa muda mrefu na kudai yamewasaidia.
Mwalongo ameyasema hayo jana baada ya hivi karibuni kuibuka utata kuhusu ubora na usalama wa mafuta hayo na kudai kuwa wao kama ATME walianza kuyatumia kama dawa kwa wateja wao siku nyingi na hawajawahi kupata malalamiko yoyote na kuwahakikishia watumiaji kuwa hayana madhara.
 
 
 
 
 Yametumika kwa zaidi ya miaka 20 na sisi tunazo kumbukumbu za wagonjwa tuliowapa mafuta hayo kama dawa na hatujawahi kupata ripoti yoyote ya madhara kwa wale waliotumia,” alisema Mwalongo.   TFDA ilitoa taarifa kwamba mafuta hayo hayafai kwa matumizi ya binadamu kwa sababu yana kiwango kikubwa cha tindikali ya mafuta aina ya cyclopropenoic fatty acids.

  Katika taarifa ya TFDA iliyotolewa juma lililopita ilisema athari zinazoweza kutokea kutokana na matumizi ya mafuta hayo ni pamoja na kuathiri vimeng’enyo vinavyosaidia katika uchakataji wa tindikali za mafuta mwilini.
  Pia ilisema ili yaweze kukidhi vigezo vya ubora na usalama ni lazima yafanyiwe usafishaji wakati wa usindikaji na kwamba kwa sasa nchini hakuna aina ya usindikaji unaofanyika wenye uwezo wa kuondoa tindikali hiyo ya cyclopropenoic fatty acids katika mafuta ya mbegu za ubuyu.
 Hata hivyo Mwalongo alikemea usambazaji holela wa mafuta hayo hasa baada ya kubainika kuwa yanatibu maradhi mbalimbali ambapo baadhi ya wajasiriamali wamekuwa wakiyasambaza wakati siyo wataalamu wa tiba asili.
  Mratibu huyo alizishauri mamlaka zinazohusika na suala zima la afya ya binadamu nchini kutoa majibu yatakayosaidia kuondoa mgawanyiko uliopo sasa kutokana na mafuta hayo badala ya kutoa taarifa za kutisha.
   Hata hivyo alipoulizwa Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Tiba Asili kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Paul Mhame, alisema hawana taarifa zozote kama kuna tafiti zimefanyika kuhusiana na matumizi ya mafuta hayo.

.MACHANGUDOA DAR WASEMA "MCHANA TUNAFUNGA, USIKU TUNAJIUZA TUPATE HELA YA FUTARI NA DAKU"....

OPARESHENI Fichua Maovu (OFM) inayoendeshwa na mapaparazi wa Global Publishers inazidi kufichua ‘madudu’ kwenye jamii, safari hii imekutana na machangu ambao wamecharuka kuendeleza biashara hiyo kwa kisingizio cha kutafuta fedha za kununulia futari.


‘Askari’ wa OFM, wiki iliyopita alifanya uchunguzi katika viunga mbalimbali maarufu kwa biashara hiyo na kukuta machangudoa wakifanya biashara yao kama inavyokuwa katika miezi ya kawaida.
Maeneo ambayo yalionekana kushamiri zaidi kwa biashara hiyo ni Barabara ya Mwananyamala Hospitali, American Chipsi, Makaburi ya Kinondoni, Viwanja vya Leaders Club, Taasisi ya Moyo, Jolly Club (Masaki), Hospitali ya Agha-Khan, New Maisha Club (Masaki) na Coco Beach.
Powered by Blogger.