Kati ya waliojinyonga ni Barnaba Venant [18] mkazi wa Mbagala ambaye alihitimu katika shule ya Sekondari ya Debrabant Mbagala ya jijini Dar es Salaam Akielezea tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Englibert Kiyondo, alisema tukio hilo lilitokea juzi, majira ya saa 4 asubuhi huko maeneo ya Nzasa, Mbagala Amefafanua kuwa, marehemu huyo alichukua uamuzi huo baada ya kutoridhishwa na matokeo yake ya mtihani wa kidato cha nne ambayo yalibainishwa alipata daraja la nne point 27 kinyume na matarajio yake Amesema kijana huyo alijinyonga kwa kutumia kamba ya manila, aliyokuwa ameitundika kwenye dari ndani ya stoo ya nyumba yao. Katika tukio lingine la aina hiyo, Michael Fidelis[19] aliyehitimu Shule ya Sekondari ya Kanyenye mjini Tabora Imedaiwa kuwa, mhitimu huyo alipogundua amepata daraja sifuri aliporudi nyumbani alichukua maamuzi ya kujinyonga hadi kufa akiwa chumbani kwake kwa kutumia kamba ya manila. Na kuacha ujumbe uliosomeka “Mama usitafute mchawi, uamuzi niliouchukua ni sababu ya matokeo yangu mabaya, nakutakia maisha mema, nisamehe sana mama.” Kufuatia matokeo hayo mabaya yaliyoleta historia vijana wengine wawili mmoja mkazi wa Kimara Temboni jijini Dar es salaam amenusurika kutoa uhai wake kwa kutoridhishwa na matokeo hayo Mwingine aliyefahamika wka jina la Hoseph Hoseah [18] mkazi wa mkoani Pwani alikimbizwa zahanati akwia aktika jaribio la kutoa uhai wake baada ya matokeo yake kuonyesha amepata daraja la nne jambo ambalo lilimfanya asiwe na raha tokea apokee matokeo hayo Imedaiwa na mmoja wa ndugu wa kijana huyo kuwa ndugu yao huyo alikuwa ni mmoja kati ya wanafunzi watano ambao shule ilikuwa ikiwatarajia wataleta sifa kwa kuleta daraja la kwanza shuleni hapo Matokeo yaliyotangazwa mwanzoni mwa wiki hii na Waziri wa Elimu yanaendelea kuleta migogoro kwa wadau huku waziri huyo akitakiwa kujiuzuru | ||
Seedr one of the best
3 years ago