Imeelezwa
kuwa Baadhi ya wazazi na walezi wilayani Kahama mkoani Shinyanga
wamekuwa wakiwazuia walimu kutoa elimu ya njia ya kujikinga na ukimwi
kwa watoto wao wa sule za msingi ikiwemo matumizi sahihi ya condom.
Hayo
yamebainika leo katika semina iliyoandaliwa na shirika la UNESCO
iliyojumisha wakuu wa shule za msingi na sekondari pamoja na mashirika
yasiyo ya kiserikali iliyofanyika katika ukumbi wa Golden Valley Mjini
Kahama.
Akichangia hoja katika semina hiyo Mwalimu mkuu wa shule
ya Msingi Korogwe Bi Ashura Rugakingira amesema kuwa wamekutana na
tatizo hilo toka kwa baadhi wazazi hao licha ya kuwa somo hilo lipo
katika mtaala wa Serikali.
Rugakingira amesema kuwa changamoto
hiyo inawafanya walimu wengi kukata tamaa ya kutoa elimu hiyo ya
kupambana na maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa wanafunzi hao.
Awali
akifungua semina hiyo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu Bi Isabela
Chilumba amewataka walimu hao kuvunja ukimya na kuwa wawazi kuzungumza
na wanafunzi wao kuhusu Maambukizi ya virusi vya ukimwi na UKIMWI.
Sambamba
na hayo Chilumba ametoa angalizo kwa wananchi kutodanganyika na takwimu
za maandishi zinazotolewa na kwamba kila mtu awe mstari wa mbele kupima
afya yake mwenyewe.
Naye Msimamizi wa mradi huo wa Elimu ya Afya
ya UKIMWI, uzazi na maadili kwa vijana kutoka UNESCO Mathius Herman
amesema lengo la mradi huo ni kujenga mahusiano rasmi kati ya Mashirika
yasiyo ya serikali na shule.
Seedr one of the best
2 years ago
No comments:
Post a Comment