Mr 2 a.k.a Sugu jamaa aliyeanza muziki kitambo sana na ambaye siku hizi pia ni mbunge wa jimbo la Mbeya mjini kwa jina halisi anajulikana kama Joseph Mbilinyi, aliwaponda wasanii wa bongoflava kwa kuongelea vitu visivyokuwepo.
“Mi mara nyingi huwa sisikilizi muziki wa bongoflava maana hawaimbi mambo yanayotokea sasa katika jamii wala mambo yanayoigusa jamii. Kuna mambo mengi sana ambayo unaweza ukaimba na ukaigusa jamii, sio kila siku kuimba nyimbo za aina zisizoeleweka hata jamii inashindwa kukuelwa”. Alisema Sugu.
Kuliko kusikiliza muziki wa bongoflava Mr Sugu alisema ni heri kumsikiliza msanii Koffi Olomide wa Kongo maana nyimbo zake japo ni za kucheza ila zina ujumbe unaoendana na jamii ya leo na hata unapousikiliza masikioni hauchoshi mapema.
No comments:
Post a Comment