MSANII WA VICHEKESHO NA MUZKI SHARO
MILIONEA AMEFARIKI LEO HUKO MUHEZA
TANGA KWA AJALI YA GARI AMBAPO NDUGU
YAKE WA KARIBU SNURA MUSHI
AMETHIBITISHA TUKIO HILO KWA NJIA YA
SIMU .....
Naye Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Afande Constatine Masawe, amethibitisha kutokea kwa kifo cha wa Sharobaro, kufuatia ajali ya gari katika kijiji cha Lusanga, Muheza, mkoani Tanga ambako ndio nyumbani kwao.......
MPAKA SASA MWILI UPO HOSPITALI TEULE YA MUHEZA ,TANGA
kikwatojr.blogspot.com imepokea habari hizi kwa mstuko na masikitiko makubwa kwani nyota ya Sharo Milionea ndiyo ilikuwa inaanza kung'ara katika anga za muziki pamoja na matangazo ya biashara, akiwa kayapumulia pumzi mpya wa ubunifu na weledi katika kupeleka ujumbe kwa watazamaji ambao wakubwa na wadogo walimpenda.
Tunaamini katika tasini ya filam na vichekesho kutakuwa na pengo kubwa sana kwani alikuwa ni mchekeshaji marufu sana na hata katika tasnia ya bongo freva pia kutakuwa na aliweza kufanya kazi kubwa na nzuri na wasanii wa hapa nchini pamoja na wasanii wa nnje na nyimbo yake ya mwisho inafahamika kama kizunguzungu akiwa amemshirikisha msanii alikiba na inafanya vizuri kwa sasa .
Wote kwa pamoja na blog hii ina wapapole mashabiki na wapenzi wote wa Sharo milionea Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi amen.
No comments:
Post a Comment