kaliya mwaka wadauuu kwa vijana wetu walio maliza darasa la saba
Msichana huyo [14] jina limehifadhiwa, ambaye alikuwa akifanya mtihani wake wa darasa la saba, alianzwa na hali ya uchungu akiwa katika chumba cha mtihani na hatimaye kujifungua mtoto
Awali ilidaiwa kuwa, mwanafunzi huyo alimuomba msimamizi wake aende msalani akajisaidie na msimamizi huyo alimruhusu, hivyo kudaiwa baada ya dakika chache alimuomba tena msimamizi huyo ruhusu aende nje lakini ilidaiwa msimamizi hakumruhusu kwa kudhani huenda mwanafunzi huyo alikuwa anafanya ujanja wa kupata majibu ya mitihani
Imedaiwa msimamizi huyo alimzuia mwanafunzi huyo asitoke lakini baadae msimamizi huyo alianza kuingiwa na wasiwasi kwa kuona binti huyo anajinyonga zaidi na kumuuliza anasumbuliwa na nini na mwanafunzi kudaiwa alimjibu anasumbuliwa na tumbo
Lakini jibu hilo halikumtosheleza msimamizi huyo kwa kuona msichana huyo anazidi kujinyonga nyonga, aliendelea kumuuliza linamuuma vipi ndipo mwanafunzi huyo alimwambia ukweli msimamizi huyo kwa kumwambia anaumwa na uchungu
Msimamizi huyo ndipo alipoanza kufanya juhudi za kutafuta msaidizi ili wamsaidie binti huyo lakini baadae binti huyo alifanikiwa kujifungua mtoto wa kiume akiwa katika chumba hicho
Taarifa hizi zimethibitishwa na uongozi wa shule ikiwemo Afisa Elimu wilayani humo akiwemo Mkurugenzi Halmashauri ya Kagera
KWA MATANGAZO MBALIMBALI KUHUSU BIASHARA YAKO USISITE KUJITANGAA KUPITIA (KIKWATOJR.BLOGSPOT.COM) WASALIANA NASI KWA SIMU NAMBA +255718991013.+25575433520
No comments:
Post a Comment