WAANDISHI WA HABARI WAANDAMANA JIJINI DAR ES SALAAM, NI KUHUSU KIFO CHA DAUDI MWANGOSI
Katibu Mkuu wa Jukwaa la Wahariri Bw. Neville Meena akizungumza mara baada ya waandishi wa habari kumaliza maadamano yao ya Amani kutoa ujumbe wao kwa jeshi la Polisi kutokana na kupoteza maisha kwa mwandishi wa habari Marehemu Daudi Mwangosi aliyeuwawa katika vurugu kati ya Polisi na Wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika kijiji cha Nyololo Mkoani Iringa hivi karibuni, Maandamano hayo yalianzia katika ofisi za kituo cha Televisheni ya Chanel Ten ambako marehemu alikuwa mwakilishi wake mkoani Iringa na kuishia katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es salaam leo asubuhi.
Waandishi wa habari mbalimbali wakitoa dukuduku zao mara baada ya kumalizika kwa maandamano hayo leo asubuhi.
kweli sasa tumeamua hatutakli tena michongooo na polisii ona sasa mpaka tumeamua kufunga midomo na kalamu zetuu hatuna tena habari na polisiii dani ya siku40 hakuna kuandika habari zoozte zinazohusu polisi angalizo kwa wale makamanda wanaopenda kuuza katika vyombo vya habari
hapa ni Waandishi wa habari wakiigiza vurugu zilizotokea mkoani Iringa ambapo Mwandishi wa habari Marehemu Daudi Mwangosi alipoteza maisha katika vurugu hizo huo ni mfano jinsi jamama alivyoteswa na polisi dar kwelii alipata tabu marahemu.
Seedr one of the best
3 years ago
No comments:
Post a Comment