MBUNGE
wa Pangani Bw Salehe Pamba ametoa msaada wa bati 80 kwa Shule ya msingi
Kilimangwido kutokana na shule hiyo kuchakaa paa lake na kuleta adha
kubwa kwa wanafunzi wa shule hiyo.
Hatua
hiyo ya Mbunge inakuja kufuatia ziara zake za hivi karibuni kubaini
uchakavu wa shule hiyo ambapo awali wanafunzi walikuwa wakinyeshewa na
mvua nyakati za masika na kudumaza kiwango cha elimu.
Alisema
juhudi hizo ni utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuwasihi
wananchi wa Pangani kuendelea kukiunga mkono chama hicho kwani
kinatekeleza ahadi zake kwa vitendo kwa lengo la kuwaletea wananchi
maendeleo.
Akikabidhi msaada huo jana kwa Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bw Albert Bukulu Mbunge huyo aliwataka wananchi wa jimbo hilo kuendelea na mshikamano walionao katika kuchangia shughuli ikiwemo elimu ili kupiga hatua kubwa za maendeleo ya jimbo hilo.
Bw
Pamba alisema wakati umefika wa wananchi kuthamini elimu kwani ndio
chimbuko la maendeleo ya jamii hiyo na kuwasisitiza wazazi umuhimu wa
kupeleka shule watoto wao.
Akipokea
msaada huo Bw Bukulu alisema umekuja wakati muafaka ambapo wanafunzi
walikuwa wakipata tabu kutokana na uchakavu wa majengo hayo na kushukuru
juhudi za MBunge huyo kuthamini elimu.
Alisema
kitendo cha Mbunge huyo kutoa msaada huo ni wazi anatambua kuwa elimu
ndio msingi wa maendeleo ya jamii na kumhakikishia kuwa msaada huo
utasaidia kuchochea kasi ya elimu katika shule hiyo.
Mbunge
huyo anaendelea na ziara yake ya kusikiliza kero za wananchi na
kuendelea kuunga mkono juhudi mbalimbali za maendeleo yanayofanywa na
wananchi wa jimbo hilo.
No comments:
Post a Comment