(Kipa wa timu ya Ruvu Shooting Benjamin Haule akipangua mkwaju wa penalti uliopigwa na Mshambuliaji wa Simba Daniel Akuffor wakati wa mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.Picha na Jackson Odoyo.)
MSHAMBULIAJI wa Simba Daniel Akuffor, amekosa penalti wakati wa mechi ya Ligi Kuu tanzania Bara, inayoendelea hivi sasa katika Uwanja wa Taifa jijini
Dar es Salaam, Mshambuliaji huyo alikosa penalti hiyo katika dakika 45 kipindi cha kwanza.
Mwamuzi wa mchezo huo Roanald Swai, aliamuru ipigwe penalt hiyo baada ya beki wa Ruvu Shooting kunawa mpira ndani ya 18.
Awali kabla ya mshambuliaji huyo raia wa Ghana kukosa penalti hiyo, Simba ilikua inaogoza kwa bao 1-0 iliyofungwa na Felix Sunzu kwa kichwa.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kila timu ikihitaji ushindi, ambapo Ruvu Shooting ndiyo iliyokuwa ya kwanza kupata goli la kusawazisha, lillilofungwa na Self Rashid dakika 75 akitokea benchi baada ya kuunasa mpira uliopigwa na beki wa Simba Nassoro Masoud (Cholo), dakika ya 80 ya mchezo mshambuliaji Kinda wa Simba aliyeingia kuchukuwa na nafasi ya Daniel Akuffor Edward Christopher alifunga bao la pili baada ya kupata pasi safi ya Mrisho Ngassa.mpaka dakika 90 Simba 2-Ruvu Shooting 1.
No comments:
Post a Comment