Blogger Widgets AWASIFIA Rooney, Van Persie kuwa WAJANJA KISOKA! | Mfaume Kikwato JR

PALACE HOTEL

PALACE HOTEL

Vumbua Hazina chini ya kizibo

Vumbua Hazina chini ya kizibo
+255788788218

BAYPORT

BAYPORT
KOPA BAYPORT

Monday, October 15, 2012

AWASIFIA Rooney, Van Persie kuwa WAJANJA KISOKA!


Beki wa Arsenal Laurent Koscielny amemshambulia Straika wa Liverpool Luis Suarez na kumwita ni mdanganyifu anaejidondosha kwa kusudi ili ahadae Marefa na kupata Penati.
Katika Wiki za hivi karibuni Suarez amekuwa akishambuliwa kutoka kila kona kuanzia kwa Meneja wa Stoke City Tony Pulis ambae mwanzoni mwa Mwezi huu alitaka Chama cha Soka England, FA, kimwadhibu Straika huyo kutoka Uruguay kwa udanganyifu.
FIFA nao, kupitia Makamu wao wa Rais, Jim Boyce, wakaingia kundini wakitaka mabadiliko ya Sheria ili FA iweze kuadhibu kwa vitendo kama hivyo baada ya kuviita ni ‘kansa katika gemu.’
Lakini Suarez hakukaa kimya na nae akajibu huku UAF, Chama cha Soka cha Uruguay, kikiingilia na kuitaka Kamati ya Maadili ya FIFA imchunguze Jim Boyce kwa kauli yake kuhusu Suarez lakini sasa nae Laurent Koscielny kabeba bango kumtuhumu Suarez.
Akiongea na Gazeti la Ufaransa L'Equipe, Koscielny alihoji: “Nani ni Fowadi ninaemchukia? Suarez. Anachosha kulinda kwa sababu ni mdanganyifu. Atakuvuta Jezi, atakupiga. Wakati wote unataka kumfyatua teke lakini unaogopa Kadi Nyekundu.”
Koscielny amekiri kuwa aliekuwa Straika wa Chelsea Didier Drogba ndie alikuwa akimvutia kwa Mastraika na amesema: “Alikuwa na nguvu, anacheza vizuri akilipa mgongo goli, mpiga vichwa mzuri na mwepesi kutafuta upenyo. Vilevile, yeye ni mlinzi wa kwanza kama tulivyoona alipowasimamisha Barcelona.”
Alipoulizwa kuhusu Wayne Rooney, Koscielny alisema: “Ni mjanja sana ingawa Robin van Persie ni mjanja zaidi. Lakini Rooney mara nyingi anashuka kwenye Kiungo. Rooney anapenda mpira na kutoa misaada kwa pasi.”

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.