Mchezaji wa timu ya Yanga ya jijini Dar es salaam akimiliki mpira mbele ya beki wa timu ya Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jioni hii jijini Dar es salaam, mpira umekwisha timu ya Yanga imeifunga Ruvu Shooting magoli 3-2, Goli la tatu la timu ya Yanga limepatikana katika kipindi cha pili cha mchezo huo baada ya kutoka uwanjani kwa mapumziko zikitoshana nguvu kwa kufungana magoli mawili kwa mawili katika kipindi cha kwanza
Mchezaji wa Yanga Jerrison Tegete akishangilia mara baada ya kufunga goli la pili katika mchezo huo na kufanya kipindi cha kwanza kumalizika timu zikitoshana nguvu kwa magoli, mpaka kipindi cha pili ambapo Yanga iliongeza goli la tatu na kufanya matokeo hayo kuwa 3-2
Seedr one of the best
3 years ago
No comments:
Post a Comment