Bunge la taifa la Libya jana lilimchagua Waziri Mkuu Mpya, huyo akiwa Waziri Mkuu Mpya wa pili kuwahi kuchaguliwa katika muda wa mwezi mmoja ambaye atakabiliana na changamoto za kuunda serikali itakayokubaliwa na mirengo mingi ya nchi hiyo. Ali Zeidan mwanadiplomasia wa zamani ambaye alielekea uhamishoni mwaka 1980 na kuwa mkosoaji wa Muammar Gaddafi kiongozi wa zamani wa Libya amechaguliwa wiki moja tu baada ya Waziri Mkuu aliyemtangulia kuachishwa kazi baada ya kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye. Musatafa Abu Shagur alifutwa kazi baada ya orodha yake ya mawaziri aliowapendekeza kukabiliwa na upinzani wa bunge na nje ya taasisi hiyo.
KWA MATANGAZO MBALIMBALI KUHUSU BIASHARA YAKO USISITE KUJITANGAA KUPITIA (KIKWATOJR.BLOGSPOT.COM) WASALIANA NASI KWA SIMU NAMBA +255718991013.+25575433520
No comments:
Post a Comment