Taarifa zilizopatikana kutoka jijini Mwanza zainasema usiku wa kuamkia leo majira ya saa 8 usiku Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Liberatus Barlow ameuawa kwa kupigwa risasi usiku huu maeneo ya hotel Tai 5, Kitangili jijini Mwanza .
Marehemu Kamanda Liberatus Barlow alifariki kabla ya kufikishwa katika hospitali ya Bugando ambapo inadaiwa alivamiwa na watu waliokuwa wamevalia mavazi ya polisi jamii ndipo aliposimamishwa na baada ya kusimama watu hao walimmiminia risasi kufuani na kupelekea kifo chake
Imeelezwa kwamba Marehemu Kamanda Liberatus Barlow alikuwa akitoka kwenye harusi na alikuwa na mtu mmoja kwenye gari aliyekuwa akimsindikiza mtu huyo ambaye ni mwanamke yeye hakudhurika na chochote katika tukio hilo.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe.Eng. Evarist Ndikilo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya uliNzi na usalama mkoani humo ameshathibitisha kutokea kwa tukio hilo la kifo cha kamanda Liberatus Barlow
No comments:
Post a Comment