Blogger Widgets hussein-machozi-kutoa-nyimbo-mpya. | Mfaume Kikwato JR

PALACE HOTEL

PALACE HOTEL

Vumbua Hazina chini ya kizibo

Vumbua Hazina chini ya kizibo
+255788788218

BAYPORT

BAYPORT
KOPA BAYPORT

Monday, October 15, 2012

hussein-machozi-kutoa-nyimbo-mpya.


NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Hussein Rashid ‘Hussen Machozi’ amesema yupo katika hatua za mwisho za uandaaji wa kibao chake kipya ambacho bado hajakipatia jina.
Akizungumza jijini Dar es Salaam alisema kutokana na ubora wa wimbo huo anapata tabu kujua aupe jina gani na anaimani mwisho wa mwezi huu utaanza kusikika redioni.
“Unajua kazi ikiwa freshi inakua tabu kutafuta jina la wimbo, hivyo nipo kwenye mchakato wa kutafuta ikibidi nitaomba ushauri kwa wasanii wengine,” alisema Hessein Machazi.
Alisema kikubwa kinachotakiwa ni sapoti kutoka kwa mashabiki na kwamba wasicheze mbali na yeye kuna vitu vingi ambavyo amewaandalia.
Mbali na kibao hicho, Hussen Machozi kwa sasa anatamba n akibao chake cha ‘Addicted’ ambacho kinafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio na runinga.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.