Blogger Widgets shirika la mfuko wa taifa wa bima ya afya lashauriwa kuongeza ufanisi katika kuboresha huduma zake | Mfaume Kikwato JR

PALACE HOTEL

PALACE HOTEL

Vumbua Hazina chini ya kizibo

Vumbua Hazina chini ya kizibo
+255788788218

BAYPORT

BAYPORT
KOPA BAYPORT

Tuesday, October 23, 2012

shirika la mfuko wa taifa wa bima ya afya lashauriwa kuongeza ufanisi katika kuboresha huduma zake

picha ni wakina mama washiriki wilayani Muheza wakiwa wanafatilia mafunzo kwa umakini
(hao pia ni mingoni  mwa  washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya unyanyasaji yanayoendeshwa kwa ufadhili wa Shirika la INUKA na SWAT )

 SHIRIKA  la Mfuko wa taifa  wa Bima ya afya limeshauriwa kuongeza ufanisi kwa  kuboresha huduma zake zaidi ili kuondoa usumbufu na malalamiko kwa wanachama wake.
Hayo yalielezwa na washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya unyanyasaji yanayoendeshwa kwa ufadhili wa Shirika la INUKA na SWAT  na kufanyika  kwenye ukumbi wa kanisa la Elimu Pentacost la Masuguru Mjini Muheza.
Washiriki hao ambao wengi wao ni walimu, walilalamika kuwa huduma za bima ya afya bado hazijatengemaa vema na kwamba kuna haja kwa wahusika kujipanga na kuhakikisha kuwa wanachama wake wanapata wanachotarajia ipasavyo.
Walidai kuwa licha ya kukatwa fedha nyingi kila mwezi lakini  fedha wanazotozwa  haziendani na huduma zinazotolewa  jambo walilolieleza kuwa linawafanya wakate tama na kujutia michango yao.
Kwamujibu wa washiriki hao ni kwamba wanalazimika kutoa michango yao kila mwezi lakini hawapati huduma wanayotarajia na badala yake wanapokwenda  hospitali wanatakiwa kulipia dawa na vipimo vingine na hivyo kupata gharama kubwa.
Mambo mengine yaliyojitokeza kwenye mafunzo hayo ni pamoja na malalamiko zidi ya Taasisi ya  Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)  Wilaya ya Muheza kudaiwa kutoa siri kwa kuwataja  kwa waharifu watu wanaojitoa kupeleka  taarifa za makosa hayo katika ofisi zao.
Aidha washiriki hao walilalamikia unyanyasaji katika jeshi la polisi.Mahakama pamoja na watendaji  mbalimbali katika maofisi ya serikali na binafsi na kwamba wamekuwa wakipata manyanyaso kwenye ajira kwa upendeleo wenye mazingira ya rushwa.
Awali mkufunzi wa mafunzo hayo Nestory Ngwega alitumia muda mwingi kueleza haki za msingi za binaadamu ambazo zisipofuatwa ndipo tendo la unyanyasaji hutokea na kwamba haki hizo zipo kwenye makundi mawili ambayo ni haki ya kikatiba na ile ya kibinaadamu ambayo haiondolewi na mtu yeyote Yule kwa nafasi yake ama uwezo wa kifedha.
Mengine yaliyojadiliwa katika mafunzo hayo ni unyanyasaji ndani ya familia na kwa wanandoa  pamoja na vyanzo vyake na jinsi ya kukabiliana navyo.




No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.