Blogger Widgets mapigano kongo sasa basi? | Mfaume Kikwato JR

PALACE HOTEL

PALACE HOTEL

Vumbua Hazina chini ya kizibo

Vumbua Hazina chini ya kizibo
+255788788218

BAYPORT

BAYPORT
KOPA BAYPORT

Monday, October 15, 2012

mapigano kongo sasa basi?


Wapinzani nchini Kongo wametaka kukomeshwa vita huko mashariki mwa nchi hiyo kufuatia kuendelea mapigano katika mkoa wa Kivu ya Kaskazini.  Lucien Mbusa Katibu Mkuu wa Harakati ya Ukombozi wa Kongo amesisitiza kwamba wapinzani nchini Kongo wanataraji kuwa Ufaransa itatumia ushawishi ilionao katika taasisi za kimataifa na hivyo kufanya juhudi za kumaliza mapigano mashariki mwa nchi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Lucien Mbusa ambaye ni mjumbe wa wapinzani katika bunge la Kongo amekutana na kufanya mazungumzo na Rais Francois Hollande wa Ufaransa mwishoni mwa kikao cha Francophone mjini Kinshasa.
Katibu Mkuu wa Harakati ya Ukombozi wa Kongo amesifu matamshi ya Rais wa Ufaransa  kuwa matokeo ya uchaguzi wa Rais wa nchi hiyo ni yenye kutia shaka,  kwamba kuna ukiukaji wa haki za binadamu na pia raia wa Kongo wanafungwa jela bila ya kuhukumiwa.

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.